waislamu - Ukurasa 30

IQNA

TEHRAN (IQNA)- Mashindano ya Qur'ani maalumu kwa wanawake wenye ulemavu wa macho yameandaliwa hivi karibuni nchini Iraq.
Habari ID: 3474528   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/11/08

TEHRAN (IQNA)- Misikiti mitatu Ufaransa imehujumiwa na watu wenye chuki dhidi ya Uislamu Jumapili katika miji ya Montlebon, Pontarlier, na Roubaix.
Habari ID: 3474527   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/11/08

TEHRAN (IQNA)- Msikiti mpya umefunguliwa hivi karibuni katika mji mkuu wa Zambia, Lusaka kwa lengo la kuwahudumia Waislamu na pia kuelimisha watu wa nchi hiyo kwa ujumla kuhusu Uislamu.
Habari ID: 3474525   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/11/06

TEHRAN (IQNA)- Jumuiya ya Waislamu katika eneo la Manawatu New Zealand imeidhinisha msikiti wa eneo hilo kutumika kama eneo la kutoa chanjo ya COVID-19 kwa watu wote.
Habari ID: 3474524   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/11/06

TEHRAN (IQNA)- Kituo cha Kiislamu cha Al Azhar nchini Misri kimekosoa uamuzi wa shule moja Uhispania kupiga marufuku vazi la Hijabu na kutaja kitendo hicho kuwa ni ubaguzi.
Habari ID: 3474523   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/11/06

TEHRAN (IQNA)- Mwenyekiti wa msikiti mmoja mjini London amebainisha masikitiko yake kuhusu kuongezeka ubaguzi na bughudha dhidi ya wanawake Waislamu.
Habari ID: 3474522   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/11/06

TEHRAN (IQNA) – Kitabu chenye anuani ya "Chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia): Kabiliana Nayo kwa Jina la Amani" kimechapishwa kwa lugha ya Kiingereza nchini Ujerumani kwa ajili ya watoto.
Habari ID: 3474515   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/11/04

TEHRAN (IQNA)- Serikali ya Ufaransa inapinga kampeni ya uhuru wa kuvaa Hijabu katika nchi za Umoja wa Ulaya jambo ambalo limepelekea video na picha za kampeni hiyo kufutwa katika mtandao wa Twitter.
Habari ID: 3474514   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/11/04

TEHRAN (IQNA)- Msikiti wa Kituo cha Kiislamu cha Al Azhar umeanza tena vdarsa za Qur'ani za kuhudhuria ana kwa ana baada ya marufuku yam waka moja na nusu kutokana na janga la COVID-19.
Habari ID: 3474513   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/11/04

TEHRAN (IQNA)- Harakati za kupigania ukombozi wa Wapalestina za Hamas na Jihad Islami zimetoa tahadhari kwa utawala wa Kizayuni wa Israel kuhusu kuwatesa mateka Wapalestina wanaoshikiliwa na utawala huo dhalimu.
Habari ID: 3474509   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/11/03

TEHRAN (IQNA)- Mwanazuoni wa ngazi za juu wa Kiislamu amelaani vikali hujuma za hivi karibuni dhidi ya Waislamu nchini India huku akitoa wito wa kuanzishwa harakati yakimataifa ya kutetea Waislamu ambao wanaishi kama jamii za waliowachache.
Habari ID: 3474495   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/31

TEHRAN (IQNA)- Mtawala wa Jimbo la Selangro nchini Malaysia ameamuru idadi ya waumini wanaoshiriki katika Sala ya Ijumaa misikitini iongezwe.
Habari ID: 3474494   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/31

TEHRAN (IQNA)- Jumuiya ya Maulamaa wa Kiislamu katika jimbo la Tripura kaskazini mashariki mwa India wameitaka serikali ya nchi hiyo ichukue hatua za kuzuia magenge ya Wahindu wenye misimamko mikali kuwashambulia Waislamu na misikiti.
Habari ID: 3474487   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/29

TEHRAN (IQNA) – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Ufaransa imetangaza mpango wa kufunga misikiti kadhaa na pia kufuta vibali vya jumuiya kadhaa za Kiislamu kwa kisingzio cha kuzuia kuenea misimamo mikali.
Habari ID: 3474484   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/28

TEHRAN (IQNA)- Wahindu wenya misimamo mikali katika jimbo la Tripura kaskazini mashariki mwa India wamewahujumu Waislamu na kuharibu misikiti minne kwa sababu ya kulipiza kisasi kutokana na kile wanachodai ni kusumbuliwa Wahindu katika nchi jirani ya Bangladesh.
Habari ID: 3474483   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/28

TEHRAN (IQNA)- Msomi wa Kiislamu nchini Misri amesema Uislamu unalipa umuhimu mkubwa suala la kulinda maeneo ya ibada hata yale ambayo si ya Waislamu.
Habari ID: 3474470   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/25

TEHRAN (IQNA)- Sherehe za kukumbuka kuzaliwa Mtume Muhammad SAW maarufu kama Milad un Nabii au Maulidi zimefanyika Jumapili jioni katika misikitini mbali mbali ya mji mkubwa zaidi Uturuki, Istanbul.
Habari ID: 3474437   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/18

TEHRAN (IQNA)- Baadhi ya manispaa nchini Uholanzi zinafanya upekuzi na upelelezi wa siri kinyume cha sheria katika misikiti na taasisi za Kiislamu kupitia mashirika binafsi ya upelelezi.
Habari ID: 3474434   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/17

TEHRAN (IQNA)- Moto ambao unashukiwa kuanzishwa na wenye chuki dhidi ya Uislamu umeharibu jengo la msikiti eneo la University Place, jimboni Washington nchini Marekani.
Habari ID: 3474420   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/13

TEHRAN (IQNA)- Mkurugenzi wa Taasisi ya Mustafa (saw) amesema kuwa wanasayansi watano Waislamu wametunukiwa tuzo ya taasisi hiyo ya mwanasayansi bora katika Ulimwengu wa Kiislamu mwaka huu wa 2021.
Habari ID: 3474418   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/13