waislamu - Ukurasa 26

IQNA

TEHRAN (IQNA)- Serikali ya Pakistan imeitaka jamii ya kimataifa, hususan Umoja wa Mataifa na mashirika husika ya kimataifa ya haki za binadamu, kuiwajibisha India kutokana na kukithiri ukiukaji wake wa haki za binadamu dhidi ya walio wachache, hasa Waislamu.
Habari ID: 3474971    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/02/24

TEHRAN (IQNA)- Wataalamu wa haki za Umoja wa Mataifa wametaka kukomeshwa kwa mashambulizi ya mtandaoni "ya kuchukiza dhidi ya wanawake na ya kimadhehebu" dhidi ya mwanahabari Muislamu nchini India, wakiomba mamlaka kuchunguza unyanyasaji huo.
Habari ID: 3474966    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/02/23

TEHRAN (IQNA)- Wabunge kadhaa nchini Kuwait wametaka wanachama wa chama tawala India, Bharatiya Janata (BJP) wapigwe marufuku kuingia nchini humo kutokana na kuhusika kwao na ukandamizaji wa Waislamu nchini India.
Habari ID: 3474955    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/02/21

TEHRAN (IQNA)- Mahakama ya Kimataifa ya Uadilifu (ICJ) leo Jumatatu inaanza kusikiliza tena kesi ya mauaji ya Waislamu wa Rohingya wa Myanmar iliyokuwa imewasilishwa na Gambia katika mahakama hiyo.
Habari ID: 3474954    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/02/21

TEHRAN (IQNA)- Bidhaa ‘Halal’ na hasa vyakula vinazidi kupata umaarufu nchini Russsia, nchi kubwa zaidi duniani.
Habari ID: 3474951    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/02/20

TEHRAN (IQNA)- Kwa mara ya kwanza katika historia ya Algeria, mwanamke mtangazaji habari amejitokeza akiwa amevaa Hijabu katika televisheni ya kitaifa.
Habari ID: 3474944    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/02/18

TEHRAN (IQNA)- Huku mzozo wa Hijabu ukiendelea kutokota katika jimbo la Karnataka nchini India, wanawake Waislamu wameandamana katika mji wa Ludhiana, jimboni Punjab kuunga mkono haki ya kuvaa Hijabu.
Habari ID: 3474924    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/02/13

TEHRAN (IQNA)- Sala ya Ijumaa haikuruhusiwa kufanywa kwa wiki ya 28 mfululizo kwenye Msikiti Mkuu huko Srinagar, katika eneo la Kashmir linalozozaniwa na ambalo linatawaliwa na India
Habari ID: 3474923    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/02/12

TEHRAN (IQNA)- Mchezaji nyota wa Manchester United, Paul Pogba aliingia kwenye mitandao ya kijamii siku ya Alhamisi na kusambaza video yenye kuwatetea wanawake Waislamu India wanaovaa Hijabu kufuatia mzozo unaoendelea kuhusu Hijab katika Jimbo la Karnataka nchini India.
Habari ID: 3474914    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/02/10

TEHRAN (IQNA)- Klipu iliyowekwa kwenye mtandao wa Twitter ikimuonyesha mwanafunzi Muislamu aliyevaa hijabu akibughudhiwa kwa maneno na genge la wahindu wenye misimamo ya kufurutu mpaka katika chuo kimoja cha jimbo la Karnataka nchini India, imezusha moto wa hasira na kuzidisha malalamiko ya kupinga marufuku ya uvaaji hijabu iliyowekwa katika taasisi za elimu za jimbo hilo.
Habari ID: 3474910    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/02/09

Msemaji wa Harakati ya Nujabaa
TEHRAN (IQNA) - Msemaji wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya al-Nujabaa ya Iraq alisisitiza kwamba Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imekuwa nchi pekee iliyosimama kidete kukabiliana na Marekani baada ya Vita vya Pili vya Dunia.
Habari ID: 3474908    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/02/08

TEHRAN (IQNA)- Umoja wa Afrika (AU) umesimamisha nafasi ya mwanachama mwangalizi ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika umoja huo hatua ambayo ni pigo kwa utawala huo unaokaliwa kwa mabavu ardhi za Palestina.
Habari ID: 3474901    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/02/07

TEHRAN (IQNA)- Msikiti mmoja katika mji mkuu wa Austira, Vienna umehujumiwa na watu wasiojulikana ikiwa ni ongezeko la chuki dhidi ya Uislamu barani Ulaya.
Habari ID: 3474893    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/02/05

TEHRAN (IQNA)- Wanawake Waislamu wanaohudumu katika Kikosi cha Gadi ya Pwani ya Ufilipino sasa wanaruhusiwa kuvaa Hijabu ikiwa ni katika jitihada za kuwahimiza wanawake Waislamu wajiunge na kikosi hicho.
Habari ID: 3474888    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/02/04

TEHRAN (IQNA) – Kituo cha Kiislamu cha Al Azhar nchini Misri kimepongeza uamuzi wa serikali ya Canada kutangaza siku maalumu ya kukabiliana na chuki dhidi ya Uislamu.
Habari ID: 3474879    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/02/01

TEHRAN (IQNA)- Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa Michelle Bachelet ameitaka jamii ya kimataifa izidishe mashinikizo kwa jeshi la Myanmar ili likomeshe kampeni yake ya ukatili na ukandamizaji dhidi ya watu wa Myanmar na kusisitiza kurejeshwa mara moja utawala wa kiraia nchini humo.
Habari ID: 3474869    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/01/30

TEHRAN (IQNA)- Waziri Mkuu wa Pakistan Imran Khan amempongeza mwenzake wa Canada kutokana na hatua yake ya kulaani chuki dhidi ya Uislamu yaani Islamophobia huku akitaka kuwepo jitihada maalumu za kukabiliana na tatizo hilo.
Habari ID: 3474868    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/01/30

TEHRAN (IQNA)-Nakala ya majaribio ya Qur'ani Tukufu iliyoandikwa kwa maandishi ya nukta nundu (braille) katika Kituo cha Kiislamu cha Al Azhar imezinduliwa katika Maoneysho ya Kimataifa ya Vitabu ya Cairo.
Habari ID: 3474859    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/01/28

TEHRAN (IQNA)- Wanafuzni Waislamu katika Shule ya Upili ya Park High mtaa wa Stanmore nchini London wanasema mwalimu mmoja shuleni hapo amewanyima idhini ya kusali Sala ya Ijumaa katika uwanja wa shule.
Habari ID: 3474857    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/01/26

TEHRAN (IQNA)- Kadhia ya chuki dhidi ya Uislamu na kubaguliwa Waislamu katika nchi za Ulaya ikiwemo Uingereza imeshika kasi katika miaka ya hivi karibuni. Chuki hizi dhidi ya Uislamu sasa zimefika hata katika ngazi rasmi za serikali.
Habari ID: 3474845    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/01/24