Muungano huo wa walimu umesisitiza kuwa utawala wa Israel ndio unaowajibika kikamilifu kwa mgogoro wa walimu na mfumo wa elimu katika ardhi zilizokaliwa kwa mabavu za Palestina.
Katika msimamo wake thabiti, muungano huo pia umeutaka utawala wa Kizayuni “kusitisha mara moja operesheni zake za kijeshi nchini Lebanon na kukomesha mpango wa kuwalazimisha wakazi kuhama kutoka maeneo ya kusini mwa nchi hiyo.” Aidha, AFT imedai kuondolewa kwa mzingiro dhidi ya bandari za Iran, kama sharti la kuwezesha kufunguliwa kwa njia ya maji ya Lango la Hormuz.
Hivi karibuni, kura ya maoni iliyotolewa imeonesha kuwa takriban asilimia 60 ya watu wazima nchini Marekani sasa wana mtazamo hasi dhidi ya utawala wa Israel. Hii inatokana na madhara mabaya na matokeo ya vita vyake vya kikatili vinavyoendelea Gaza na uchokozi wake wa hivi karibuni dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
/3498358