IQNA

Mashindano ya Qur'ani

Mashindano ya Qur'ani kwa wanawake yalifanyika Dar es-Salaam Tanzania

20:43 - August 14, 2024
Habari ID: 3479280
IQNA - Mashindano ya Qur'ani kwa wanawake yamefanika katika mji wa Dar es Salaam, Tanzania wikiendi iliyopita.

Taasisi ya Aisha Sururu iliandaa hafla hiyo, ambayo sherehe zake za kufunga zilihudhuriwa na wabunge kadhaa.

Washindani walishindana katika kuhifadhi Qur'ani Tukufu katika ngazi 8 (kuhifadhi Juzuu 1,  Juzuu tatu, Juzuu tano, Juzuu saba, Juzuu kumi, Juzuu 15, Juzuu 20, Juzuu 25 na Juzuu zote 30 za Qur'ani Tukufu

Washindi wa safu tatu za juu katika kila ngazi walitunukiwa katika hafla hiyo iliyofana.

Haya yalikuwa mashindano ya pili ya Qur'ani kwa wanawake jijini Dar es-Salaam ndani ya miezi miwili.

Ya awali ilifanyika Julai na yaliandaliwa na Taasisi ya Umm al-Mumineen na kuhudhuriwa na maafisa kadhaa wa serikali pamoja na viongozi mbali mbali wa kidini.

Jiji hilo pia litaandaa mashindano ya kimataifa ya Qur'ani kwa wanawake wa nchi za Afrika mwezi Septemba.

Quran Competition for Women Held in Tanzania’s Dar es-Salaam

Kutakuwa na washiriki kutoka nchi 11 za Afrika watakaoshindana katika mashindano yajayo ya kimataifa.

Katika miaka ya hivi karibuni Tanzania imekuwa mwenyeji wa mashindano kadhaa ya kitaifa na kimataifa ya Qur'ani Tukufu.

Habari zinazohusiana
captcha