IQNA

Mashindano ya Qur'ani

Fainali ya Mashindano ya Kimataifa ya Qur’ani ya Makka yakamilika

19:06 - August 17, 2024
Habari ID: 3479290
IQNA – Sehemu ya mwisho  ya Toleo la 44 la Mashindano ya Kimataifa ya Mfalme Abdulaziz ya Kuhifadhi , Kusoma na Kutafsiri Qur'ani Tukufu huko Makka imekamilika huko Makka.

Walioingia fainali ni kutoka Yemen, Iran, Burkina Faso, Palestina, Hong Kong, Marekani, Burundi, Russia, Kongo na Ethiopia.

Walikuwa wamechaguliwa kutoka kwa washiriki 174 kutoka nchi 123 ili kushiriki katika duru ya mwisho.

Mashindano hayo yalikamilika Ijumaa asubuhi na washindi wa safu za juu watatangazwa katika hafla ya kufunga kwenye Msikiti Mkuu wa Makka siku ya Jumatano.

Wizara ya Masuala ya Kiislamu ya Saudia, imeandaa mashindano hayo katika Msikiti Mkuu wa Makka kati ya Safar 5 na 17, 1446 AH (Agosti 9 na 21, 2024).

Mohammad Mehdi Rezaei na Mohammad Hossein Behzadfar wanawakilisha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika hafla ya kimataifa ya Qur'ani.

4232056

Habari zinazohusiana
captcha