Walioingia fainali ni kutoka Yemen, Iran, Burkina Faso, Palestina, Hong Kong, Marekani, Burundi, Russia, Kongo na Ethiopia.
Walikuwa wamechaguliwa kutoka kwa washiriki 174 kutoka nchi 123 ili kushiriki katika duru ya mwisho.
Mashindano hayo yalikamilika Ijumaa asubuhi na washindi wa safu za juu watatangazwa katika hafla ya kufunga kwenye Msikiti Mkuu wa Makka siku ya Jumatano.
Wizara ya Masuala ya Kiislamu ya Saudia, imeandaa mashindano hayo katika Msikiti Mkuu wa Makka kati ya Safar 5 na 17, 1446 AH (Agosti 9 na 21, 2024).
Mohammad Mehdi Rezaei na Mohammad Hossein Behzadfar wanawakilisha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika hafla ya kimataifa ya Qur'ani.
4232056