IQNA

Umrah

Wanafunzi 4500 wa Iran kutekeleza Hija ndogo ya Umrah

23:29 - December 04, 2024
Habari ID: 3479855
IQNA - Wanafunzi wapatao 4,50 wa vyuo vikuu vya Iran wameteuliwa kupitia shindano ili kuweza kushiriki Hija ndogo ya Umra.

Katika hafla hiyo iliyofanyika Jumanne katika Chuo Kikuu cha Tehran, iliyohudhuriwa na viongozi wa kidini na wasomi, akiwemo Hujjatul Islam Mostafa Rostami, Mkuu wa Ofisi ya Mwakilishi wa Kiongozi katika Vyuo Vikuu na Alireza Bayat, Mkuu wa Jumuiya ya Hijja na Hija, maafisa walisisitiza umuhimu wa kuwasaidia wanafunzi kutekelelza ibada ya Umrah.

Rostani amewashauri washiriki kujiandaa na ibada ya Umrah kwa kusoma kuhusu kanuni na umhuhimu wa ibada hii.

Bayat ameitaja Umrah kuwa ibada ya kiroho na kuongeza kuwa. "Kuwepo Umrah kwa akili changa kunaongeza hisia za kujitolea katika maeneo kama Makka na Madina," alisema.

Wanafunzi waliochaguliwa wataondoka  nchini kupitia  viwanja vya ndege vinne vilivyoteuliwa vyaTehran, Isfahan, Kerman, na Mashhad. Bayat amewataka wanafunzi kuzingatia kanuni nchini Saudi Arabia, kama vile vikwazo vya upigaji picha na matumizi ya mitandao ya kijamii.

Habari zinazohusiana
Kishikizo: umrah iran
captcha