IQNA

Umrah

Huduma ya uhifadhi wa mizigo yaanzishwa kwa Mahujaji wa Umrah huko Makka

22:04 - December 28, 2024
Habari ID: 3479966
IQNA – Mamlaka za Makka zimetangaza kuanzishwa kwa huduma za kuhifadhi mizigo kwa mahujaji wa Umrah, lengo likiwa ni kuwarahisishia wageni wa Msikiti Mkuu wa Makka.

Mamlaka Kuu ya Utunzaji wa Mambo ya Msikiti Mkuu  wa Makka na Msikiti wa Mtume jijini Madina imefichua kuwa maeneo ya kuhifadhi mizigo sasa yanafanya kazi katika maeneo mawili muhimu: mashariki mwa Msikiti Mkuu karibu na Maktaba ya Makka, na magharibi karibu na Lango la 64. Kulingana na Shirika la Habari la Saudia (SPA), Mahujaji wanatakiwa kuwasilisha vibali vyao rasmi kupitia programu ya simu ya Nusuk ili kupata huduma ya kuhifadhi mizigo. Vituo hivyo vimeundwa kuhifadhi mizigo inayozidi uzito wa kilo 7. Mizigo inatunzwa kwa muda usiozidi masaa manne, na bidhaa kama vile vitu vya thamani, bidhaa zilizopigwa marufuku, chakula, na dawa haziruhusiwi. Mahujaji pia wanapaswa kuhifadhi na kuwasilisha tikiti wakati wa kuchukua mizigo yao. Mamlaka hiyo imeonyesha mipango ya kupanua huduma hii polepole katika maeneo yote yanayozunguka Msikiti Mkuu.

3491234

Kishikizo: makkah umrah
captcha