Katika tamko lake, CFCM imekosoa matamshi ya kisiasa na ya vyombo vya habari dhidi ya wanawake Waislamu.” Baraza hilo limebainisha kuwa ongezeko la ukosefu wa usalama, matusi ya maneno, na mashambulizi ya kimwili dhidi ya wanawake wa Kiislamu, linatokana hali hii na mijadala ya umma inayochochea mgawanyiko.
Baraza hilo limekosoa sera zinazoelezwa kuwa ni za kukuza uhuru au usekula, likisema kwamba mara nyingi zinachukua mtazamo wa “kiburi na hatari” kuhusu wanawake Waislamu.
Limepinga juhudi za kutunga sheria dhidi ya uwepo wa kidini, likisema kwamba hatua hizo zinakiuka kanuni za usawa na usekula.
Baraza hilo pia limkemea wanasiasa na vyombo vya habari kutumia busara, uwiano, na uwajibikaji, likisisitiza kwamba masuala haya yasichukuliwe kama nafasi ya michezo ya kisiasa. CFCM liliitaka jamii kuweka mshikamano wa kitaifa mbele ya hoja za kugawanya, na kusisitiza uhuru na heshima ya wanawake wa Kiislamu.
3492515