Lengo ni kuvutia ushiriki wa jumuiya ya Qur’an, hususan wanazuoni na wasanii, ili maonyesho haya ya kimataifa yawe na hadhi na uzuri zaidi.
Kwa mujibu wa Idara ya Mahusiano ya Umma na Habari ya Kituo Kikuu cha Qur’an na Etrat cha Wizara ya Utamaduni na Muongozo wa Kiislamu Iran, washiriki wanaweza kupiga kura kuchagua kauli mbiu kutoka miongoni mwa chaguo nane zifuatazo:
Aya zinakuita
Kufahamu aya, kufanikisha vilele
Qur’an na Etrat; mhimili wa umoja
Pamoja na Qur’an hadi mbinguni
Qur’an, Kitabu cha mwamko
Qur’an chanzo cha maisha na matumaini
Sisi na Qur’an
Kutoka Aya hadi Kioo
Muda wa kushiriki utaisha tarehe 10 Januari 2026, na wanaotaka kushiriki wanaweza kujiandikisha kupitia tovuti www.iqfa.ir.
Baada ya kura kukamilika, kauli mbiu bora itatangazwa rasmi kama kauli mbiu ya Maonyesho 33 ya Kimataifa ya Qur’an Tukufu, na washiriki 10 watazawadiwa tuzo muhimu kupitia droo.
Maonyesho haya hufanyika kila mwaka katika mwezi mtukufu wa Ramadhani chini ya Wizara ya Utamaduni na Muongozo wa Kiislamu ya Iran. Yakiambatana na vipindi maalumu, warsha za kielimu, makongamano ya Qur’an, na shughuli mahsusi kwa watoto na vijana, maonyesho haya yanalenga kueneza dhana na shughuli za Qur’an.
Aidha, jukwaa hili hutumika kuonyesha mafanikio ya hivi karibuni ya Qur’an nchini Iran pamoja na bidhaa mbalimbali zinazohusiana na kuendeleza Kitabu Kitukufu.
3495985