waislamu - Ukurasa 3

IQNA

IQNA – Mashirika kadhaa ya Kiislamu nchini Ufaransa yamekosoa taasisi ya utafiti wa maoni ya wananchi, IFOP, kwa kile walichokiita upendeleo wa wazi na kuvunja viwango vya maadili ya kitaaluma.
Habari ID: 3481564   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/25

IQNA – Mkutano wa 38 wa Kimataifa wa Waislamu wa Amerika ya Kusini na Karibiani unafanyika nchini Brazil, ukikusanya viongozi wa Kiislamu kujadili mada ya vijana Waislamu katika enzi ya akili mnemba (AI).
Habari ID: 3481553   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/22

IQNA – Kamati ya Masuala ya Katiba ya Ureno imeamua kuwa pendekezo la kuzuia ufadhili wa umma kwa ujenzi wa misikiti halina msingi wa kikatiba.
Habari ID: 3481549   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/21

IQNA – Baada ya tukio la uhalifu wa chuki lililoripotiwa ambapo dada Muislamu alivamiwa na kufuatwa karibu na Chuo Kikuu cha Columbia kwa sababu ya kuvaa niqab, taasisi hiyo imetoa tamko la kulaani shambulio hilo hadharani.
Habari ID: 3481522   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/16

IQNA – Mradi wa kutafsiri Qur'an kwa lugha ya Rohingya umeanzishwa katika mazingira ambapo Waislamu wa Rohingya wamekuwa wakilengwa na dhulma na kufukuzwa kutoka ardhi yao kwa miongo kadhaa. Lengo lake ni kuziba pengo la maarifa ya Kiislamu na kupambana na ukandamizaji wa lugha ya Rohingya.
Habari ID: 3481493   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/09

IQNA-Katika ripoti mpya iliyotolewa na taasisi ya utafiti ya Uswidi, imebainika kuwa idadi kubwa ya wanafunzi Waislamu wamekuwa wakihama shule kutokana na kukumbwa na ubaguzi wa rangi na chuki dhidi ya Uislamu.
Habari ID: 3481482   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/07

IQNA-Zohran Mamdani mbunge Muislamu amechaguliwa kuwa Meya wa 111 wa jiji la New York, mtu wa kwanza mwenye asili ya Asia Kusini na wa kwanza aliyezaliwa barani Afrika kuongoza jiji kubwa zaidi nchini Marekani.
Habari ID: 3481471   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/05

IQNA – Imamu Mkuu wa Kituo cha Kiislamu cha Al-Azhar nchini Misri, Sheikh Ahmad al-Tayyib, amesema kuwa dunia inakumbwa na machafuko na ukosefu wa mantiki, hali ambayo chanzo chake ni kupuuzwa kwa maadili ya kidini na kiutu.
Habari ID: 3481456   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/03

IQNA – Kupitia ukurasa wake wa Facebook, mhadhiri wa chuo kikuu kutoka Misri, Sayed Sharara, amefungua dirisha la kipekee kuonesha maisha ya Waislamu nchini Japani.
Habari ID: 3481455   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/03

IQNA – Polisi nchini New Zealand wanafanya uchunguzi kuhusu tishio la bomu lililolenga Msikiti wa Kilbirnie uliopo Wellington, hali iliyosababisha kusitishwa kwa shughuli zote za msikiti huo kwa muda.
Habari ID: 3481411   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/25

IQNA – Mtandao wa Mazungumzo ya Kiislamu nchini Norway (Islamic Dialogue Network) umezindua tovuti ya kwanza ya kitaifa ya kupambana na chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia), iitwayo stoppmuslimhat.no.
Habari ID: 3481403   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/23

IQNA- Kufuatia ongezeko kubwa la uhalifu wa chuki dhidi ya Waislamu nchini Uingereza, serikali inatarajiwa kutangaza ufafanuzi mpya wa neno “'Chuki Dhidi ya Uislamu' (Islamophobia)”—ambapo huenda likabadilishwa na kuwa “chuki dhidi ya Waislamu.”
Habari ID: 3481402   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/23

IQNA – Jumuiya ya Waislamu wa jiji la Winnipeg, mji mkuu wa jimbo la Manitoba nchini Kanada (Canada), walikusanyika mwishoni mwa wiki hii kusherehekea ufunguzi rasmi wa msikiti mpya katika jiji hilo.
Habari ID: 3481392   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/21

IQNA – Kituo cha Al-Azhar cha Kupambana na Itikadi Kali kimetoa onyo kali kuhusu matumizi mabaya ya teknolojia ya Akili Mnemba (AI) katika kuchochea chuki dhidi ya Waislamu nchini India.
Habari ID: 3481391   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/21

IQNA – "Misikiti katika Uislamu" ni jina la maonyesho ya sanaa yaliyozinduliwa katika Msikiti Mkuu wa Paris, mji mkuu wa Ufaransa.
Habari ID: 3481379   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/18

IQNA – Maktaba ya Kitume ya Vatican imetenga eneo dogo kwa ajili ya watafiti Waislamu kuswali wanapoitembelea.
Habari ID: 3481369   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/15

IQNA – Tume ya Haki za Binadamu ya Australia imeanzisha uchunguzi kufuatia malalamiko dhidi ya Baraza la Wahindu la Australia, likiwemo Rais wake Sai Paravastu na Mkuu wa Idara ya Habari Neelima Paravastu, wakidaiwa kujihusisha mara kwa mara na matamshi ya chuki dhidi ya Uislamu kuanzia Mei 2024 hadi Julai 2025.
Habari ID: 3481273   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/23

IQNA – Mwakilishi wa Misri ameibuka mshindi wa kwanza katika mashindano ya kimataifa ya usomaji wa Qur'ani ya mataifa ya BRICS yaliyofanyika nchini Brazil.
Habari ID: 3481199   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/08

IQNA – Mashambulizi mawili ya hivi karibuni dhidi ya msikiti mmoja huko Greater Manchester nchini Uingereza yamewaacha waumini wakihisi kutokuwa salama, kwa mujibu wa Imam wake.
Habari ID: 3481189   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/06

Ayatullah Mohammad Hassan Akhtari
IQNA – Miongoni mwa malengo makuu ya shughuli na mikakati ya Wiki ya Umoja wa Kiislamu mwaka huu ni kuvuta hisia za dunia kuhusu dhulma na masaibu yanayowakumba ndugu zetu Wapalestina, afisa mmoja amesema.
Habari ID: 3481182   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/04