qurani tukufu - Ukurasa 24

IQNA

IQNA – Jukwaa la kielimu la Qur’ani kwa ajili ya wasiozungumza Kiarabu linazinduliwa nchini Saudi Arabia.
Habari ID: 3481069   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/11

IQNA – Katika Ukanda wa Gaza uliokumbwa na vita, dada watatu wa Kipalestina wamekamilisha kuhifadhi Qur’ani Tukufu yote, licha ya kuvumilia mashambulizi ya kijeshi ya Kizayuni, uhamisho wa kulazimishwa, na njaa kali.
Habari ID: 3481067   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/11

IQNA – Wawakilishi wawili kutoka Malaysia wametwaa ubingwa katika Mashindano ya 65 ya Kimataifa ya Kusoma na kuhifadhi Qur’ani Tukufu ya Malaysia (MTHQA) ya 65, kila mmoja katika kipengele chake husika.
Habari ID: 3481061   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/10

IQNA – Waziri Mkuu wa Malaysia amesema kuwa serikali yake itatenga ufadhili wa ziada kwa Yayasan Restu ili kuwezesha tafsiri ya Qur’ani Tukufu katika lugha nyengine 30, na hivyo kupanua zaidi upeo wa ujumbe wake wa ulimwengu.
Habari ID: 3481060   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/09

IQNA – Mufti Mkuu wa Misri amesema kuwa akili mnemba (Artificial Intelligence – AI) haina mamlaka ya kutoa maamuzi ya Kiislamu au fatwa.
Habari ID: 3481058   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/09

IQNA – Mashindano ya 65 ya Kimataifa ya Qur’ani ya Malaysia (MTHQA), yameimarika kwa mtazamo wa viwango ambapo majaji wamepongeza mahadhi na uhifadhi ulio bora zaidi.
Habari ID: 3481056   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/09

IQNA – Tuzo ya Kimataifa ya Qur’ani Tukufu ya Dubai imetangaza matokeo ya mchujo wa awali, ambapo washiriki 525 wamechaguliwa kuendelea katika toleo la 28 la mashindano hayo.
Habari ID: 3481055   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/09

IQNA – Katika ufunguzi wa Kongamano la Dunia la Qur’ani 2025 jijini Kuala Lumpur, Malaysia, wito umetolewa wa kuifanya Qur’ani kuwa mwongozo wa kina katika utungaji sera, elimu, na mikakati ya kiuchumi na isiwe ni ya usomaji na kuhifadhi pekee.
Habari ID: 3481052   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/09

IQNA – Mashindano ya tatu ya kila mwaka ya kuhifadhi Qur’ani yanayoandaliwa na Msikiti Mkuu wa Al-Azhar nchini Misri yatafanyika kwa ushirikiano na benki ya Kiislamu.
Habari ID: 3481046   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/06

IQNA – Wizara ya Wakfu na Mwongozo ya Yemen imetangaza kuwa itafanya mtihani maalum kwa ajili ya kuwachagua wawakilishi wa nchi hiyo watakaoshiriki katika mashindano ya kimataifa ya Qur'ani katika mataifa mbalimbali.
Habari ID: 3481045   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/06

IQNA – Malaysia imezidisha juhudi za kuitangaza Qur'an Tukufu kama mwongozo wa maisha yenye maadili, kwa lengo la kulea kizazi chenye msingi imara wa tabia njema na uchamungu.
Habari ID: 3481041   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/06

IQNA – Mfululizo wa miradi ya kipekee ya Qur'an Tukufu imezinduliwa huko Makkah kwa lengo la kuihudumia Kitabu Kitukufu cha Mwenyezi Mungu.
Habari ID: 3481040   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/05

IQNA – Shule ya Qur'ani ya Novi Pazar nchini Serbia ni miongoni mwa vituo muhimu zaidi vya elimu ya Qur'ani katika eneo la Balkan, ikijitahidi kufufua utambulisho wa Kiislamu miongoni mwa Waislamu wa eneo hilo na kuwafundisha Qur'ani Tukufu pamoja na tafsiri yake kwa wenye nia.
Habari ID: 3481029   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/02

IQNA – Washindi wa upande wa wanaume katika awamu ya kimkoa ya Mashindano ya 48 ya Kitaifa ya Qur’ani Tukufu nchini Iran, yaliyofanyika Tehran, wametangazwa rasmi katika hafla ya kufunga mashindano hayo na kukabidhiwa vyeti vya heshima pamoja na zawadi za fedha.
Habari ID: 3481028   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/01

IQNA – Wizara ya Awqaf na Masuala ya Kiislamu nchini Qatar inaendesha darasa maalum la kiangazi la Qur’ani Tukufu kwa lengo la kuimarisha uwezo wa kuhifadhi na kusoma Qur’ani miongoni mwa wanafunzi.
Habari ID: 3481027   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/01

IQNA – Mwanazuoni mmoja wa Kiislamu kutoka Nigeria amezindua mradi wa kipekee wa tarjuma ya Qur’ani Tukufu kwa lengo la kuwafikishia ujumbe wa Allah kwa jamii zinazozungumza Kiyoruba duniani kote.
Habari ID: 3481025   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/01

IQNA – Mwanaume mwenye umri wa miaka 27 nchini Ufaransa amehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja gerezani kwa kitendo cha kuvunjia heshima Qur'ani, Kitabu Kitakatifu cha Uislamu.
Habari ID: 3481024   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/01

IQNA – Kundi la walimu na maqarii mashuhuri wa Qur’ani kutoka Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limeandika barua ya wazi kwa maqari wa Misri, likiwataka wachukue msimamo dhabiti dhidi ya ukatili wa utawala wa Kizayuni huko Gaza na kusimama pamoja na watu wanyonge wa eneo hilo.
Habari ID: 3481022   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/07/30

IQNA – Afisa mmoja kutoka Wizara ya Elimu ya Iran amesema kuwa shule 1,200 za kuhifadhi Qur’ani zinapangwa kuzinduliwa nchini ili kusaidia mpango wa kuwafundisha wahifadhi milioni 10 wa Qur’ani.
Habari ID: 3481018   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/07/30

IQNA-Kozi ya kiangazi ya wanawake ya kuhifadhi Qur’ani Tukufu katika Msikiti Mtukufu wa Masjid al-Haram, Makkah, imekamilika kwa mafanikio, ambapo washiriki zaidi ya 1,600 wametimiza masharti ya programu hiyo.
Habari ID: 3481013   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/07/28