Jinai za Israel
IQNA – Jumla ya wanawake na watoto 90 wa Kipalestina waliachiliwa kutoka magereza ya kuogofya ya Israel mapema Jumatatu kama sehemu ya kubadilishana wafungwa iliyohusishwa na makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Hamas na utawala haramu wa Israel.
Habari ID: 3480083 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/01/20
Muqawama
IQNA – Mkuu wa Idara ya Mahakama ya Iran amesema kuwa utawala wa Kizayuni umelazimika kusitisha mapigano na Harakati ya Kiislamu ya Ukombozi wa Palestina, Hamas, huko kwa sababu ya udhaifu na kukata tamaa. Hii ni moja ya heshima za mstari wa mbele wa upinzani, alisema Hujjatul-Islam Gholam Hossein Mohseni Ejei, akihutubia mkutano wa 13 wa "Gaza; Alama ya Muqawama" jijini Tehran.
Habari ID: 3480073 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/01/18
Kadhia ya Palestina
IQNA-Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas imesema kuwa, kulazimika utawala wa Kizayuni kukubali kusimamisha vita na kukomesha mauaji yake ya kimbari dhidi ya wananchi wa Ghaza, ni matunda ya Muqawama (mapambano ya Kiislamu) na kusimama imara wananchi wa ukanda huo kwa zaidi ya miezi 15.
Habari ID: 3480062 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/01/16
Muqawama
IQNA- Harakati ya Mapambano ya Kiislamu Palestina (Hamas) imeidhinisha pendekezo la kusimamisha mapigano kwa Ukanda wa Gaza ambayo yamefikiwa kwa upatanishi wa Misri na Qatar.
Habari ID: 3480060 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/01/15
Muqawama
IQNA-Jeshi la Yemen limetangaza kwamba limeilenga kwa mafanikio Wizara ya Vita ya utawala haamu wa Israel na kuitwanga kwa kombora la balestiki.
Habari ID: 3480052 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/01/14
Jinai za Israel
IQNA-Katika mwaka uliomalizika wa 2024, wanajeshi wa utawala wa Kiziayuni wa Israel walibomoa kikamilifu Misikiti 815 na kuharibu mingine 151 katika Ukanda wa Ghaza. Hayo yameelezwa katika ripoti iliyotolewa na Wizara ya Wakfu na Masuala ya Dini ya Palestina.
Habari ID: 3480011 Tarehe ya kuchapishwa : 2025/01/06
Muqawama
IQNA-Kiongozi wa Harakati ya Muqawama ya Ansarullah ya Yemen amesema kuwa, kitendo cha utawala wa Israel cha kunyakua ardhi zaidi ya Syria wa hivi karibuni baada ya kuangushwa serikali ya nchi hiyo ni sehemu ya mpango wa utawala huo wa Kizayuni unaoitwa 'Israeli Kubwa'.
Habari ID: 3479924 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/12/20
Jinai
IQNA-Siku moja baada ya vikosi vya ulinzi vya Yemen kushambulia mji mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel Tel Aviv kwa kombora la 'hypersonic, la Palestina 2 ndege za kivita za Marekani na Uingereza zimeshambulia maeneo kadhaa ya Harakati ya Ansarullah katika mji mkuu wa Yemen, Sana'a
Habari ID: 3479914 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/12/17
Jinai za Israel
IQNA-Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limepitisha kwa wingi mkubwa wa kura maazimio mawili, moja la kutaka kusitishwa kwa mapigano mara moja katika Ukanda wa Ghaza na la pili la kuutaka utawala wa Kizayuni wa Israel uondoe marufuku yake kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuwahudumia Wakimbizi wa Palestina, UNRWA.
Habari ID: 3479893 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/12/12
Jinai za Israel
IQNA - Milipuko iliyosikika Jumatatu usiku karibu na madhabahu takatifu ya Hadhrat Zeynab (SA) katika kitongoji cha Damascus ilisababishwa na shambulio la bomu la ndege za kivita za Israel, duru zilisema.
Habari ID: 3479887 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/12/10
Uchambuzi
IQNA - Utawala wa Kizayuni wa Israel unalenga kwa nguvu zote kusambaratisha mhimili wa muqawama Asia Magharibi na kutenganisha makundi ya muqawama huko Iraq, Syria na Lebanon, amesema mchambuzi wa masuala ya kisiasa wa Iraq.
Habari ID: 3479870 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/12/07
IQNA - Maelfu ya watu wa Lebanon wanarejea makwao kusini mwa Lebanon baada ya kusitishwa kwa mapigano kati ya utawala haramu wa Israel na Harakati Hizbullah. Mapatano hayo yalivikiwa Jumatano iliyopita.
Habari ID: 3479836 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/12/02
Kadhia ya Palestina
IQNA--Kwa mwaka wa pili mfululizo Siku ya Kimataifa ya Mshikamano na Wananchi wa Palestina imeadhimishwa huku Gaza ikiendelea kuwa chini ya hujuma kubwa ya mashambulizi ya utawala wa Kizayuni sambamba na kuenezwa propaganda na taarifa ghushi za utawala huo
Habari ID: 3479829 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/11/30
Muqawama (Mapambano ya Kiislamu)
IQNA- Hatimaye baada ya miezi 14 ya vita vikali kati ya utawala wa Kizayuni wa Israel na Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon, usitishaji vita wa siku 60 umeanza kutekelezwa asubuhi ya leo (Jumatano) baina ya pande hizo mbili.
Habari ID: 3479815 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/11/27
Jinai za Israel
IQNA-Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei ametoa wito wa kuhukumiwa kifo Waziri Mkuu wa utawala haramu wa Israel, Benjamin Netanyahu, ambaye waranti ya kukamatwa kwake imetolewa na Mahakama ya kimataifa ya Uhalifu (ICC) huku utawala huo ukiendeleza mauaji ya kimbari ya utawala huo ghasibu huko Gaza na nchini Lebanon.
Habari ID: 3479809 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/11/25
Muqawama
IQNA-Kiongozi wa Hizbullah amesema harakati hiyo ya muqawama ya Lebanon iko tayari kupigana vita vya muda mrefu dhidi ya utawala ghasibu wa Israel, na kwamba jibu lao kwa mashambulizi ya hivi karibuni ya anga dhidi ya Beirut litakuwa kulenga katikati mwa Tel Aviv.
Habari ID: 3479786 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/11/21
Watetezi wa Qur'ani
IQNA-Kitendo cha hivi punde zaidi cha kuvunjiwa heshima Qur'ani na askari wa utawala haramu wa Israel huko Gaza kimelaaniwa na watu wengi, ikiwa ni pamoja na kundi kubwa zaidi la kutetea Waislamu nchini Marekani ambalo lilitaka Waislamu wachukuliwe hatua dhidi ya hatua hizo za kusikitisha.
Habari ID: 3479780 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/11/20
Jinai za Israel
IQNA - Picha inayosambaa mtandaoni inamuonyesha mwanajeshi wa utawala katili wa Israel akivunjia heshima nakala ya Qur'ani Tukufu huko Gaza ikiwa ni kitendo cha hivi karibuni cha uadui wa jeshi hilo dhidi ya Waislamu duniani.
Habari ID: 3479774 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/11/19
Jinai za Israel
IQNA - Kundi la waandamanaji wanaouunga mkono utawala haramu wa Israel walimnyanyasa na kukandamiza Mbunge wa Uingereza Jeremy Corbyn nje ya ukumbi wa mkutano ambapo mkutano wa kupinga ubaguzi wa rangi ulikuwa unafanyika.
Habari ID: 3479762 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/11/17
Diplomasia
IQNA - Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema utawala wa Marekani unaomaliza muda wake unatarajiwa kutumia muda uliobakia madarakani kukomesha hujuma za Israel huko Gaza na Lebanon.
Habari ID: 3479738 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/11/11