IQNA

Waumini wanaaswa wasilete watoto katika Msikiti Mkuu wa Makkah wakati kuna msongamano

21:03 - March 24, 2025
Habari ID: 3480429
IQNA – Waumini wametakiwa kutowaleta watoto wadogo katika Msikiti Mkuu wa Makkah, Masjid al Haram, wakati wa siku za mwisho za mwezi mtukufu  Ramadhani. Hii ni kutokana na eneo hili takatifu kushuhudia ongezeko kubwa la umini

Mwezi wa Ramadhani, ambao unatarajiwa kumalizika mwaka huu tarehe 29 Machi, mara nyingi huwa msimu wa kilele wa Umrah au Hija ndogo katika Msikiti Mkuu wa Makaa, ambao ni eneo takatifu zaidi katika Uislamu.

Kituo cha Kitaifa cha Operesheni za Usalama cha Wizara ya Mambo ya Ndani ya Saudi Arabia kimewasihi waumini kuepuka kuleta Watoto wadogo msikitini wakati kilele cha ibada katika Msikiti Mkuu kwa sababu za usalama.

Shirika hilo lilisisitiza umuhimu wa kufuata miongozo ya usalama ili kuhakikisha faraja wakati wa kuongezeka kwa idadi ya wageni wakati wa sala katika msikiti, ambao ni sehemu muhimu kwa Waislamu kutoka kote duniani.

Mamlaka Kuu ya Utunzaji wa Misikiti Mitakatifu Miwili, kwa upande mwingine, ilisema inatoa mazingira salama kwa watoto katika vituo vya utunzaji watoto vilivyo na vifaa vizuri.

Vituo hivi vinatoa huduma masaa 24 ili kutoa mazingira salama na yenye furaha kwa watoto, na kuwapa wazazi fursa ya kutekeleza ibada zao katika Msikiti Mkuu kwa utulivu.

"Watoto wenu wapo mikononi salama," ilisema taarifa ya shirika hilo kwa wazazi, ikirejelea vituo hivi.

Mamilioni ya Waislamu kutoka ndani na nje ya Saudi Arabia huenda kwenye maeneo takatifu zaidi ya Uislamu ya Msikiti Mkuu wa Makkah na Msikiti wa Mtume katika mji wa Madina kwa ajili ya ibada za kina katika Ramadhani.

3492481

captcha