IQNA

Kozi Maalum ya Wahifadhi wa Qur’ani Yazinduliwa katika Masjid an-Nabawi Madina

17:53 - April 17, 2026
Habari ID: 3482146
IQNA – Katika juhudi za kuhakikisha kuwa wahifadhi wa Qur’ani Tukufu wanaendelea kuihifadhi kwa uthabiti wa muda mrefu, Msikiti wa Mtume SAW (Masjid an-Nabawi) umezindua programu mpya na makini ya muraja‘a kupitia idara ya halaqa za kuhifadhi Qur’ani.

Idara ya halaqa za kuhifadhi Qur’ani imetangaza kuanzishwa kwa programu hii ya muraja‘a ya kina kwa wahifadhi, ikiwa ni sehemu ya juhudi zake zinazoendelea za kuwasaidia wale waliokwisha ihifadhi Qur’ani Tukufu.

Idara hiyo imeeleza kuwa programu inapatikana katika viwango mbalimbali, vikiwemo muraja‘a ya Qur’ani nzima, juzuu 20, na juzuu 10, ili washiriki waweze kujiunga kulingana na kiwango chao cha sasa cha hifdh.

Programu hiyo itafanyika tarehe 17 hadi 18 Aprili katika eneo la halaqa za kuhifadhi Qur’ani ndani ya Msikiti wa Mtume, karibu na Lango la 22.

Wale wanaopenda wanahimizwa kunufaika na fursa hii, ambayo inalenga kuimarisha na kukamilisha hifdh ya Qur’ani Tukufu.

3497121

Habari zinazohusiana
captcha