
Wazo la mradi huu lilianza Vatican mwaka 2015 katika mazungumzo kuhusu Nabii Isa (AS). Alisoma aya za Surah Maryam na tafsiri wake alilia, jambo lililomgusa na kumfanya atambue haja ya kufafanua ukweli wa Qur’ani Tukufu kuhusu Nabii Isa (AS) au Yesu kama anavyojulikana miongoni mwa Wakristo. Baadaye aliandika kitabu Ukweli Kamili Kuhusu Kristo, Isa bin Maryam, kilichotafsiriwa kwa lugha kadhaa na kujadiliwa Ulaya.
Baada ya Isa (AS), aliandika kuhusu Nuh (AS) na Adam (AS), kutokana na kuwa Qur’ani Tukufu inatoa mifano mikubwa ya kuigwa. Lengo la ensaiklopidia hii ni kuwaunganisha watu na Qur’ani Tukufu, kuimarisha Tauhidi, kueleza njia za manabii katika kupambana na batili, na kutoa mifano ya vitendo ya kufuata.
Hadithi za Qur’anI zinatoa suluhisho halisi kwa changamoto za binadamu wa kisasa. Yusuf (AS) ni mfano wa subira na ushindi dhidi ya vishawishi; Ayyub (AS) ni mfano wa subira njema; Yunus (AS) ni mfano wa kutafuta hifadhi kwa Allah; Ibrahim (AS) ni mfano wa kupambana na ibada ya sanamu kwa hoja; Musa (AS) ni mfano wa kupinga dhulma na kuwaokoa wanyonge.
Maisha ya manabii wote ni mwonekano wa kanuni kubwa ya maadili. Qur’anI Tukufu inataja Ummah kama taifa moja la Tauhidi, heshima na haki. Hadithi hizi zinaunda utambulisho wa kimaadili unaokabiliana na dhulma na maovu. Utambulisho huu unaonekana kwa Daud (AS), Suleiman (AS), Zakariya (AS), Hud (AS), na Yusuf (AS).
Al-Salabi alisema kitabu hiki kinasaidia wahubiri na wanafunzi kufikisha ujumbe wa manabii kwa njia ya Qur’ani Tukufu na hadith sahihi. Ingawa hadithi zote zimemgusa, ile ya Musa (AS) imemgusa zaidi kwa sababu ya mapambano yake dhidi ya Firauni na juhudi za kuwaokoa wanyonge. Mwisho, alimuomba Allah kitabu hiki kiwe na manufaa kwa wote, kwani hadithi za Qur’ani Tukufu ni sehemu ya kumbukumbu ya binadamu katika historia.
3495836