IQNA

Wawakilishi wa Iran washinda katika Mashindano ya Kimataifa ya Qur'ani ya Lebanon

15:15 - February 16, 2026
Habari ID: 3481946
IQNA – Washiriki kutoka Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wamefanikiwa kushinda nafasi ya kwanza na ya pili katika mashindano ya kimataifa ya Qur'ani Tukufu yajulikanayo kama “Al‑Sadiq Al‑Amin”, yaliyofanyika nchini Lebanon.

Mohammad Reza Jafarpour alitwaa tuzo ya kwanza katika kipengele cha Hifdh ya Qurani Tukufu yote, huku Mehdi Rashtbari akipata nafasi ya pili katika kipengele cha usomaji (tilawa) wa Qur'ani.

Hatua ya mwisho ya mashindano hayo ya kimataifa ya Qur'ani ilifanyika kwa ana kwa ana mjini Beirut tarehe 13 na 14 Februari, baada ya hatua za awali kufanyika kwa njia ya mtandao.

Mashindano hayo yaliandaliwa na Kituo cha Kitamaduni cha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Lebanon, kwa ushirikiano na Jumuiya ya Qur'ani Tukufu ya Lebanon.

Jopo la majaji lilijumuisha wanazuoni na wataalamu mashuhuri wa Qur'ani, akiwemo Hujjatul Islam Mohammad Haji Abolqasem na Ali Mehrabi kutoka Iran; Adel Khalil, Sheikh Mohammad Al‑Saleh na Haitham Ayyash kutoka Lebanon; Sheikh Khairuddin Al‑Hadi kutoka Iraq; Kamal Qada kutoka Algeria; pamoja na Sheikh Abdel Nasser Harak kutoka Misri.

Kwa mujibu wa vigezo vya majaji, katika kipengele cha usomaji wa Qur'ani, tathmini ilijumuisha:

  • Kuzingatia kanuni za Tajwid (alama 40)
  • Sauti (Sawt) (alama 15)
  • Waqf na Ibtida (alama 20)
  • Lahaja na maqamat (tone) (alama 25)

Katika kipengele cha Hifdh, vigezo vilikuwa:

  • Ubora wa kuhifadhi Qur'ani (alama 70)
  • Ubora wa usomaji (alama 30)

Ushindi huu unaakisi kiwango cha juu cha taaluma ya Qurani miongoni mwa washiriki wa Iran, na unaimarisha nafasi ya mashindano haya kama jukwaa muhimu la kukuza uhusiano wa Qurani na mshikamano wa kiroho miongoni mwa Waislamu wa mataifa mbalimbali.

3496431

captcha