
Ofisi ya Haki za Binadamu ya UN siku ya Alhamisi imesema kuwa video ya tukio hilo ni “ya kuudhi kupita kiasi” na ikatoa wasiwasi kuhusu uwezekano wa kukamatwa na kuzuiliwa kinyume cha sheria katika maji ya kimataifa.
“Kile kinachoonekana katika video hii ni cha kushangaza na cha kuudhi,” msemaji Ravina Shamdasani amesema katika taarifa.
Alikuwa akirejea video iliyoshirikiwa na waziri mwenye misimamo mikali katika utawala wa Israel, Itamar Ben‑Gvir, inayoonyesha wanaharakati waliokamatwa wakiwa wamefungwa kwa mikononi na kulazimishwa kupiga magoti baada ya kukamatwa na askari katili wa Israel katika maji ya kimataifa.
Msafara wa meli za misaada wa Global Sumud ulisema Jumanne kwamba meli zote 50 za msafara wake zilitekwa na Israel baada ya kushambuliwa katika maji ya kimataifa katika kitendo ambacho kimetajwa kuwa ni uharamia wa kiserikali.
Shamdasani amesema ofisi yake “ina wasiwasi mkubwa juu ya hali inayowakumba mamia ya wanaharakati walioelekea Gaza waliokamatwa na vikosi vya Israel wakiwa ndani ya meli zenye bendera za kigeni katika maji ya kimataifa, na kisha kushikiliwa na jeshi la majini la Israel, kufuatia kile kinachoonekana kuwa ni kukamatwa na kuzuiliwa kinyume cha sheria.”
Amesema kuwa kutangaza kuwa kosa kutoa msaada wa kuokoa maisha ni “jambo lisilokubalika kabisa.”
3497551