IQNA

Maombolezo

Qari Karim Mansouri akisoma aya kwenye Khitma ya Qur'ani ya 'Mashahidi wa Huduma' Iran

22:40 - May 26, 2024
Habari ID: 3478889
IQNA - Qari mashuhuri wa Iran Ustadh Karim Mansouri alisoma aya ya 100 ya Surah An-Nisa na vile vile aya za mwisho za Surah Al-Fajr katika kikao cha Khitma ya Qur'ani kwa ajili ya hayati shahidi Rais Ebrahim Raisi wa Iran na mashahidi wenzake.

Hafla hiyo ilifanyika katika katika Ukumbi wa Husseiniya ya Imam Khomeini  mjini Tehran tarehe 25 Mei 2024, ambapo Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei alijumuika na wananchi wa matabaka mbali mbali, maafisa wa serikali na mabalozi wa nchi za kigeni.

Helikopta iliyokuwa imembeba Raisi Raisi, Waziri wa Mambo ya Nje Amir-Abdollahian, kiongozi wa Swala ya Ijumaa ya Tabriz Ayatollah Mohammad Ali Al-e-Hashem, Gavana wa Azarbaijan Mashariki Malek Rahmati, kamanda wa kikosi cha usalama cha rais, marubani wawili na walinzi ilianguka mkoa wa kaskazini-magharibi wa Azarbaijan Mashariki mnamo Mei 19, 2024. Miili yao ilipatikana siku ya Jumatatu baada ya msako wa usiku mzima katika eneo lililokuwa na hali mbaya ya hewa.

Iran iliadhimisha siku tano za maombolezo ya kitaifa. Shahidi Raisi Raisi alizikwa katika Haram Takatifu ya Imam Ridha  (AS) huko Mashhad naye Shahidi Amir-Abdollahian akazikwa kwenye Haram Takatifu ya Hadhra Abdul  Adhim  Hassani (AS) huko Rey, kusini mwa Tehran.

 

Habari zinazohusiana
captcha