qurani tukufu - Ukurasa 5

IQNA

IQNA – Hafla maalumu ilifanyika nchini Yemen kuwaenzi wanafunzi 200 waliokamilisha masomo yao katika vikao vya Qur’ani vilivyoendeshwa misikitini katika kitongoji cha Madhbah, Wilaya ya Maeen.
Habari ID: 3481939    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/15

IQNA – Mutawalli wa Haram Tukufu ya Imam Hussein (AS) amesisitiza kuwa kulea na kukuza haiba au shakhsia ya Kiislamu kwa mujibu wa Qur’ani Tukufu ni msingi wa kujenga jamii kamilifu na yenye fadhila.
Habari ID: 3481935    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/14

IQNA – Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran yamegeuka kuwa mfano hai wa kuunganisha dini, maisha ya kijamii na maendeleo katika ulimwengu wa kisasa, amesema mchambuzi mmoja wa masuala ya kisiasa kutoka Lebanon.
Habari ID: 3481925    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/12

IQNA – Kituo cha Sheikha Hessa Bint Ali Al Khalifa cha Kuhifadhi Qur’ani Tukufu na Kufundisha Sayansi za Qur’ani kimefunguliwa rasmi kwa ajili ya wanawake katika eneo la Al‑Bustain, mkoa wa Muharraq, nchini Bahrain.
Habari ID: 3481924    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/12

IQNA – Shambulio la ndege zisizo na rubani au droni lililolenga msikiti na kituo cha kuhifadhi Qur’ani katika jimbo la Kordofan Kaskazini nchini Sudan limesababisha vifo vya watoto watatu na kujeruhi wengine 13.
Habari ID: 3481921    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/12

IQNA – Ingawa kipindi cha vipaji vya Qur’ani cha Misri “Dawlat El‑Tilawah" bado hakijafikia hatua ya fainali, Maqari au wasomaji wawili waliobainika kwa umahiri wao katika kipindi hicho walitunukiwa zawadi katika hafla rasmi iliyofanyika katika Chuo Kikuu cha Cairo.
Habari ID: 3481917    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/11

IQNA – Mashindano maalum ya Qur'ani yaliyobuniwa mahsusi kwa watu wenye usonji wa Down yamefanyika kwa mafanikio makubwa mjini Benghazi, Libya, yakilenga usomaji wa Qurani, hifadhi ya Qurani, na Adhana.
Habari ID: 3481915    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/10

IQNA – Jumuiya ya Qur'ani ya Iran imesisitiza kuwa vita kuu duniani hadi leo bado ni vita juu ya Qur'ani, ikisema kuwa hali ya sasa ya maendeleo ya kimataifa inaonyesha wazi kuwa wakati umefika kwa mazungumzo na fikra za Qur'ani kujitokeza kwa nguvu katika uwanja wa umma.
Habari ID: 3481913    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/10

IQNA – Omar Ali Awad ametangazwa na kutunukiwa tuzo ya “Tawi la Dhahabu” katika shindano la vipaji vya Qur’ani lijulikanalo kama “Dawlet El Telawa (Hali ya Usomaji)” nchini Misri.
Habari ID: 3481903    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/08

IQNA – Meya wa Jiji la New York, Zahran Mamdani, ametetea agizo lake linaloweka mipaka kwa ukamataji unaofanywa na maafisa wa Idara ya Uhamiaji na Forodha ya Marekani (ICE), akieleza kuwa ulinzi wa wahamiaji si suala la kisera pekee, bali ni wajibu wa kimaadili unaochochewa na mafundisho ya Qur’ani Tukufu na Hijra ya Mtume Muhammad (rehema na amani ziwe juu yake) kwenda Madina.
Habari ID: 3481900    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/08

IQNA-Malaysia inaendelea kutumia diplomasia ya kitamaduni na kidini kwa kusambaza nakala 40,000 za Qur’ani Tukufu zenye tarjuma katika lugha mbali mbali huko Marekani na Afrika Magharibi.
Habari ID: 3481898    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/07

IQNA-Malaysia iko mbioni kuanzisha chuo kikuu maalumu kwa elimu za Qur’ani, kufuatia ridhaa ya Sultan wa Pahang ya kubadilisha jina la taasisi ya elimu iliyopo tayari.
Habari ID: 3481897    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/07

IQNA – Wageni wa Jumba la Makumbusho ya Qur’ani Tukufu katika Wilaya ya Kitamaduni ya Ḥirā’, mjini Makka, sasa wanayo fursa ya kushuhudia turathi adhimu iliyovunja rekodi ya dunia: nakala ya Qur’ani Tukufu iliyoandikwa kwa mkono, iliyo kubwa zaidi kuliko zote duniani, ambayo sasa inaonyeshwa rasmi kwa umma.
Habari ID: 3481893    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/05

Mwokozi katika Qur’ani Tukufu / 1
IQNA – Aya ya 55 ya Surat An-Nur inaeleza juu ya jamii tukufu ambayo bado haijawahi kutimia kikamilifu katika ulimwengu huu, wala haiwezi kutekelezwa juu ya jamii yoyote ile isipokuwa ile itakayoundwa kwa baraka ya kudhihiri kwa Imamu Mahdi (AS).
Habari ID: 3481892    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/05

IQNA — Toleo la tisa la Mashindano ya Kimataifa ya Kuhifadhi Qur’ani na Ibtihal ya Port Said limehitimishwa, ambapo washiriki kutoka Misri wameibuka kidedea kwa kushinda nafasi ya kwanza katika makundi yote matatu ya mashindano hayo.
Habari ID: 3481884    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/03

IQNA – Mfungwa mmoja katika mkoa wa Balıkesir, nchini Uturuki, amefikia daraja ya Hafidh, baada ya kuhifadhi Qur’ani Tukufu yote kupitia mpango wa elimu ya magerezani unaoungwa mkono na serikali.
Habari ID: 3481870    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/30

IQNA – Yatima arobaini na wanane nchini Jordan wamepata thawabu tukufu ya safari ya Umrah iliyogharamiwa kikamilifu, baada ya kung’ara katika mashindano ya kuhifadhi Qur’ani Tukufu.
Habari ID: 3481869    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/30

IQNA – Hafla maalumu ilifanyika katika Msikiti wa Barduşit mjini Pristina, mji mkuu wa Kosovo, kwa lengo la kuwaenzi wanafunzi 80 wa kike wa Qur’ani walioshiriki katika duru za masomo ya Qur’ani Tukufu.
Habari ID: 3481866    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/29

IQNA – Chuo Kikuu cha Jamia Millia Islamia (JMI) mjini New Delhi, India, kilizindua rasmi kongamano kubwa la kimataifa la siku tatu siku ya Jumatano, likiwakusanya wasomi na wanazuoni kutoka pembe mbalimbali za dunia ili kuchambua kwa kina uhusiano hai kati ya mafundisho ya Qur’ani Tukufu na maendeleo ya sayansi ya kisasa.
Habari ID: 3481865    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/29

IQNA – Mlipuko mkubwa wa fataki uliomkumba Eiman Najwan Anwar Fuad ulimnyang’anya uwezo wa kuona na kuharibu mikono yake akiwa na umri wa miaka 22.
Habari ID: 3481863    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/29