صفحه نخست

فعالیت قرآنی

سیاست و اقتصاد

بین الملل

معارف

اجتماعی

فرهنگی

شعب استانی

چندرسانه ای

عکس

آذربایجان شرقی

آذربایجان غربی

اردبیل

اصفهان

البرز

ایلام

خراسان جنوبی

بوشهر

چهارمحال و بختیاری

خراسان رضوی

خراسان شمالی

سمنان

خوزستان

زنجان

سیستان و بلوچستان

فارس

قزوین

قم

کردستان

کرمان

کرمانشاه

کهگیلویه و بویر احمد

گلستان

گیلان

لرستان

مازندران

مرکزی

هرمزگان

همدان

یزد

بازار

صفحات داخلی

کد خبر: ۱۳۰۶۱۰۲
تاریخ انتشار : ۲۹ مهر ۱۳۹۲ - ۱۷:۰۸

Sheikh Mkuu wa al al Azhar nchini Misri amelaani vikali shambulizi la kigaidi lililofanywa na watu wasiojulikana dhidi ya kanisa la al Adh'raa katika wilaya ya Giza.



Taarifa iliyotolewa na Sheikh Ahmad al Tayyib imesema, shambulizi la kigaidi lililolenga Kanisa la al Adh'raa wilayani Giza ni kitendo cha jinai kinachopingana na dini na maadili.


Mufti wa Misri Shauqi Allam pia ametoa taarifa akilaani shambulizi hilo na kutangaza kuwa, dini ya Uislamu inaharamisha na kukataza kuvunjiwa heshima au kuharibiwa makanisa, kulipua mabomu na kuua watu wanaokuwamo na kuzusha hali ya hofu baina ya wafuasi wa makanisa hayo.


Mufti wa Misri amewataka Waislamu na Wakristo wa Misri kushikamana kwa ajili ya kuzima fitina zinazoenezwa na baadhi ya watu nchini Misri.


Makundi mbalimbali ya kisiasa ya Misri pia yamelaani shambulizi lililofanywa na watu wasiojulikana dhidi ya Kanisa la al Adh'raa.


Watu wasiojulikana jana walishambulia Kanisa la Sayyida al Adh'raa katika wilaya ya Giza wakati Makopti walipokuwa wakitoka nje ya kanisa hilo na kuua watu wanne aliokuwa katika sherehe ya harusi. Watu wengine 18 walijeruhiwa. 1305939