Ripoti zinasema kuwa, zaidi ya walowezi 125 wamevamia viwanja vya Msikiti wa al Aqsa mapema leo Jumapili wakipewa himaya na ulinzi na jeshi la Israel na wamewapiga na kuwaudhi Waislamu wa Kipalestina waliokuwa wakielekea eneo hilo kwa ajili ya ibada.
Vilevile wanajeshi wa Israel wamewatia nguvuni wahudumu 5 wa Msikiti wa al Aqsa na vijana watatu wa Kipalestina na kuwaachia wawili miongoni mwao baadaye.
Machafuko mapya katika viwanja vya Msikiti wa al Aqsa yameanza baada ya wanajeshi wa Israel kumkamata na kumpiga kijana moja wa Kipalestina aliyekuwa kati ya raia waliokuwa wakitekeleza ibada ya Swala na kuwapiga wenzake waliojaribu kumtetea.
Mapema leo pia jeshi la Israel liliweka vizuri vya barabarani na kuwazuia Wapalestina kuelekea kwenye Msikiti wa al Aqsa kwa ajili ya ibada. Makumi ya Wapalestina pia wametiwa nguvuni katika machafuko hayo.