Katika taarifa, jumuiya hiyo ilisisitiza kwamba hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi ya qari yeyote, maarufu au asiyejulikana, ambaye anakidharau Kitabu Kitakatifu, tovuti ya Bawaba Ruz al-Yusuf iliripoti.
Mapema, Mkuu wa jumuiya hiyo Sheikh Mohamed Hashad alitoa wito kwa watu kuwaalika makari wenye uwezo katika programu zao za usomaji wa Qur'ani na kutafuta msaada kutoka kwa jumuiya katika suala hili.
Haya yanajiri baada ya qari aitwaye Samir Antaer kujibu simu yake ya mkono ya mobile wakati akiwa anasoma Qur’ani.
Alikuwa akisoma Qur’ani Tuku katika ibada ya maombolezo wakati simu yake ya mkononi iliita. Aliacha kisomo na kujibu simu yake kabla ya kuendelea na kisomo.
Hatua yake hiyo imeibua shutuma nyingi nchini Misri. Hashad alionyesha kukerwa kwake sana na hatua hiyo na akamwita Antar ili amkanye kuhusu tabia yake hiyo.
Alisema alichofanya qari hakikufaa kutokana na hadhi tukufu ya Qur’ani.
4235253