IQNA-Idadi ya matukio na vitendo vya chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu nchini Uingereza iliongezeka kufikia kiwango cha juu zaidi mwaka 2024. Hayo ni kwa mujibu wa taarifa zilizokusanywa na shirika la ufuatiliaji la Tell MAMA, ambalo limesema vita vya Gaza "vimechochea kupita kiasi" masuala ya chuki dhidi ya Waislamu kwenye mitandao ya kijamii.

Kwa mujibu wa tasisi hiyo, kuongezeka kwa matukio ya chuki dhidi ya Waislamu yanayotokana na uenezaji chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia) kumehusishwa pia na mauaji ya wasichana watatu katika mji wa kaskazini mwa Uingereza wa Southport yaliyotokea wakati wa msimu wa joto uliopita, wakati taarifa za uwongo ziliposambazwa kwenye mitandao ya kijamii kwamba aliyehusika na mauaji hayo, -ambaye tangu wakati huo anatumikia kifungo cha miaka 52 jela-, alikuwa mhamiaji Muislamu mwenye itikadi kali, na hivyo kusababisha machafuko ya kibaguzi yaliyohusisha vikundi vya siasa kali za mrengo wa kulia na vile vinavyopinga uhamiaji nchini Uingereza.
3491918