IQNA

Mahujaji wa Umrah watembelea Kituo cha Uchapishaji wa Qur’ani Tukufu cha Madina

16:51 - July 13, 2026
Habari ID: 3482477
IQNA – Kundi la waumini wanaotekeleza Hija ndogo ya Umrah lilitembelea siku ya Jumamosi Kituo cha Mfalme Fahd cha Uchapishaji wa Qur’ani Tukufu mjini Madina.

Mahujaji hao walikuwa ni kundi la kwanza la wageni chini ya Mpango wa Hija, Umrah na Ziara wa Mlinzi wa Misikiti Miwili Mitukufu.

Waumini hao 250 , waliowakilisha nchi 16 za bara la Asia, walipata fursa ya kuzungukia kituo hicho na kujionea kwa karibu taratibu za uchapishaji wa hali ya juu, tafsiri, pamoja na usambazaji wa kimataifa wa misahafu ya Qur’ani Tukufu.

Mwishoni mwa ziara hiyo, uongozi wa kituo uliwakabidhi wageni hao nakala za Qur’ani Tukufu pamoja na tafsiri za maana zake.

Kituo cha Mfalme Fahd cha Uchapishaji wa Qur’ani Tukufu, kilichopo Madina, kinajulikana kwa uzalishaji wake mkubwa wa nakala za Qur’ani Tukufu.

Kilianzishwa mwaka 1984, na kwa wastani huzalisha takribani nakala milioni 10 za Qur’ani kila mwaka, zikiwemo tafsiri katika lugha nyingi kama vile Kiingereza, Kiswahili, Kiindonesia, Kirusi, Kijapani, Kifarsi, Kiurdu, Kibengali na Kikorea.

3498220

captcha