Mahujaji hao walikuwa ni kundi la kwanza la wageni chini ya Mpango wa Hija, Umrah na Ziara wa Mlinzi wa Misikiti Miwili Mitukufu.
Waumini hao 250 , waliowakilisha nchi 16 za bara la Asia, walipata fursa ya kuzungukia kituo hicho na kujionea kwa karibu taratibu za uchapishaji wa hali ya juu, tafsiri, pamoja na usambazaji wa kimataifa wa misahafu ya Qur’ani Tukufu.
Mwishoni mwa ziara hiyo, uongozi wa kituo uliwakabidhi wageni hao nakala za Qur’ani Tukufu pamoja na tafsiri za maana zake.
Kituo cha Mfalme Fahd cha Uchapishaji wa Qur’ani Tukufu, kilichopo Madina, kinajulikana kwa uzalishaji wake mkubwa wa nakala za Qur’ani Tukufu.
Kilianzishwa mwaka 1984, na kwa wastani huzalisha takribani nakala milioni 10 za Qur’ani kila mwaka, zikiwemo tafsiri katika lugha nyingi kama vile Kiingereza, Kiswahili, Kiindonesia, Kirusi, Kijapani, Kifarsi, Kiurdu, Kibengali na Kikorea.
3498220