iqna

IQNA

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA) - Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa mauaji ya watu laki moja katika shambulizi la bomu la nyuklia la Marekani huko Hiroshima ni kielelezo cha tabia na hulka ya kibeberu ya jeshi la nchi hiyo na utovu wa maadili na dini wa Marekani.
Habari ID: 3473043    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/08/07

TEHRAN (IQNA) - Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametoa ujumbe kufuatia tukio la mlipuko katika bandari ya Beirut nchini Lebanon na kutangaza kuwa pamoja na serikali na wananchi wa nchi hiyo katika kipindi hiki kigumu.
Habari ID: 3473039    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/08/06

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA)- Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema: Tiba ya vikwazo ni kuutumia ipasavyo uwezo na fursa za ndani, na si kusalimu amri mbele ya matakwa ya Marekani.
Habari ID: 3473020    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/07/31

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA) - Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema: "Katika matukio ya sasa ya Marekani na harakati ya kupinga ubaguzi wa rangi iliyopo, msimamo wetu thabiti ni wa kuwaunga mkono wananchi na kulaani mwenendo wa kikatili wa utawala wa ubaguzi wa rangi wa nchi hiyo."
Habari ID: 3473011    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/07/29

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA) - Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, matokeo ya mashinikizo ya maadui dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu yatakuwa ni kuchezea kipigo maadui hao kutoka kwa taifa la Iran na kulazimika kurudi nyuma.
Habari ID: 3472905    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/06/27

TEHRAN (IQNA) - Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametoa mkono wa pole kufuatia kuaga dunia Katibu Mkuu wa zamani wa Harakati ya Jihadu Islami ya Palestina, Ramadhan Abdullah Shalah.
Habari ID: 3472847    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/06/08

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA) - Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema, kuwasha moto wa vita katika nchi kadhaa ikiwemo Afghanistan, Iraq na Syria ni miongoni mwa sababu za kuchukiwa Marekani na akabainisha kwamba, Wamarekani wanaeleza kinagaubaga kuwa 'tumeweka vikosi Syria kwa sababu kuna mafuta'; lakini bila shaka hawataweza kubaki, si Iraq wala Syria. Ni lazima waondoke huko na hakuna shaka kuwa wataondoshwa tu.
Habari ID: 3472777    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/05/18

TEHRAN (IQNA)- Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametuma ujumbe maalumu wa kulishukuru na kulipongeza utendaji kazi wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu IRGC.
Habari ID: 3472692    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/04/22

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA)- Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema Marekani haiaminiwi hata kidogo na kuongeza kuwa: "Wakati Marekani inatuhumiwa kutegeneza kirusi cha corona, ni mwanadamu yupi mwenye akili atakubali msaada wa nchi hiyo."
Habari ID: 3472592    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/03/22

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu katika ujumbe wa Nairuzi*
TEHRAN (IQNA) - Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameutaja mwaka mpya wa Kiirani wa 1399 Hijria Shamsia ulioanza leo nchini Iran kuwa ni Mwaka wa Ustawi Mkubwa katika Uzalishaji na kusema: Hatua kubwa ya uzalishaji inapaswa kuleta mabadiliko yanayohisika katika maisha ya wananchi.
Habari ID: 3472584    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/03/20

TEHRAN (IQNA)- Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Alhamisi usiku alitoa amri kwa Meja Jenerali Mohammad Baqeri Mkuu wa Kamandi ya Majeshi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kutaka kamandi hiyo iunde 'Kituo cha Afya na Matibabu' kwa lengo la kukabiliana na ugonjwa wa COVID-19 ambao ni maarufu kama kirusi cha Corona.
Habari ID: 3472561    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/03/13

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA) - Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameafiki pendekezo kuwa, wafanyakazi wa sekta ya afya wanaofariki wakiwa katika mstari wa mbele wa kupambana na ugonjwa wa COVID-19 maarufu kama Corona wahesabiwe kuwa ni mashahidi.
Habari ID: 3472553    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/03/11

TEHRAN (IQNA) - Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametoa maelekezo muhimu kuhusiana na mradhi yaliyoenea ya COVID-19 yanayosababishwa na kirusi cha corona humu nchini Iran.
Habari ID: 3472527    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/03/03

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi
TEHRAN (IQNA) - Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amewashukuru wananchi kwa kuufuzu kwa kiwango cha kuridhisha mtihani mkubwa wa uchaguzi na kuweza kuzima propaganda za kila upande za maadui na kutumia kwao vibaya suala hilo na akasisitiza kwamba: Taifa zima linapaswa kuwa macho na kujiweka tayari kukabiliana na njama za adui zinazolenga kutoa pigo kwa mihimili tofauti ya nchi.
Habari ID: 3472499    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/02/23

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA) - Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuhusu mahudhurio makubwa ya wananchi imara wa Iran katika maandamano ya Bahman 22, na katika kuusindikiza mwili wa shahidi Luteni Jenerali Qassem Soleimani, aliyekuwa Mkuu wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu, kwamba uthabiti mkubwa wa taifa la Iran wa kuyakabili mashinikizo makubwa na ya kinyama ya Marekani umewastaajabisha wafuatiliaji wa masuala ya kimataifa.
Habari ID: 3472474    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/02/15

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
THERAN (IQNA) - Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema pigo la Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran (IRGC) kwa adhama ya Marekani ni jambo ambalo limepelekea nchi hiyo ifedheheke na kuongeza kuwa: "Pigo hilo kubwa na lenye nguvu haliwezi kufidiwa kwa chochote na hivyo hatua ya hivi karibuni ya Marekani ya kuongeza vikwazo haiwezi kuondoa fedheha hiyo."
Habari ID: 3472379    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/17

Kiongozi Muadhamu katika mkutano na Amir wa Qatar:
TEHRAN (IQNA) - Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Khamenei amesema: Mazingira ya eneo yalivyo hivi sasa yanahitaji zaidi kuliko ya kabla yake kuimarishwa mawasiliano kati ya nchi za eneo na kutokubali kuathiriwa na chokochoko za maajinabi.
Habari ID: 3472366    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/13

TEHRAN (IQNA) - Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameeleza masikitiko yake kuhusiana na mkasa wa ndege ya abiria ya Ukraine iliyotunguliwa kimakosa karibu na mji wa Tehran ambapo sambamba na kusema kuwa, yuko pamoja na familia zilizopoteza ndugu zao katika mkasa huo wa kuhuzunisha ametoa amri ya kufanyika uchunguzi kuhusiana na uwezekano wa kufanyika uzembe na wahusika kuchukuliwa hatua.
Habari ID: 3472362    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/11

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA) -Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, mashambulio ya makombora yaliyofanywa na Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu IRGC katika kambi mbili za Marekani nchini Iraq ni kibao cha uso tu alichopigwa adui huyo.
Habari ID: 3472353    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/08

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA) - Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Ali Khamenei ametuma salamu za rambirambi kutokana na kuuliwa shahidi Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Luteni Jenerali Qassem Suleimani na kusema kuwa: Kisasi kikali kinawasubiri watenda jinai ambao mikono yao michafu imemwaga damu yake na mashahidi wengine katika shambulizi la usiku wa kuamkia leo.
Habari ID: 3472329    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/03