"Katika mashambulizi 36 ambayo Ofisi ya Haki za Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa ilithibitisha taarifa zake, vifo vilivyorekodiwa kufikia sasa ni vya wanawake na watoto tu", ameeleza Shamdasani.
Taarifa ya uchunguzi huo imetolewa wakati mashambulizi mapya ya kinyama ya utawala wa Kizayuni dhidi ya Ghaza hadi sasa yameshawaua shahidi zaidi ya Wapalestina 1,500 tangu jeshi la utawala huo ghasibu livunje makubaliano ya usitishaji vita Machi 18.
Utawala wa Kizayuni wa Israel umeweka vizuizi kamili kwenye eneo la pwani ya Palestina na kuzuia kuingizwa kitu chochote ndani ya Ghaza, na kupelekea Umoja wa Mataifa na mashirika ya haki za binadamu kuonya kwamba chakula, maji, dawa na vifaa vingine muhimu vinamalizika haraka katika eneo hilo lililowekewa mzingiro.
Mapema wiki hii, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres alitangaza kuwa, “zaidi ya mwezi mzima umepita bila ya hata tone moja la msaada kufika Ghaza”.
Guterres alilitaja eneo la Ukanda wa Ghaza lililowekewa mzingiro na utawala wa Kizayuni wa Israel kuwa ni “uwanja wa mauaji,” na akatoa wito wa kusitishwa mapigano mara moja na kwa sura ya kudumu na kuruhusiwa misaada ya kibinadamu kuingizwa kwenye eneo hilo bila vizuizi.
Kwa ujumla tokea utawala haramu wa Israel uanzishe mauaji ya kimbari dhidi ya Gaza Oktoba 7 mwaka 2023, utawala huo umeua Wapalestina wasiopungua 51, 000 wengi wakiwa ni wanawake na watoto.
3492655