Kwa Ruqaiya Ridhai, mshiriki wa mwisho katika Mashindano ya 47 ya Kitaifa ya Qur'ani ya Iran, kuhifadhi Qur'ani imekuwa safari ya maisha ya kujitolea, nidhamu, na msaada wa kifamilia.
Bi. Ridhai ameyasema hayo katika mazungumzo mafupi na Shirika la Habari za Qur'ani la Kimataifa (IQNA) pembizoni mwa ushiriki wake katika mashindano ya kitaifa ya Iran huko Tabriz siku ya Ijumaa.
Akiwa alianza safari yake ya Qur’ani akiwa na umri mdogo wa miaka mitano, Ridhai anamsifu mama yake kwa kumtia moyo.
"Mafanikio yangu katika nyanja ya Qur'ani yanatokana na familia yangu, hasa mama yangu, ambaye alinihimiza kujiandikisha katika madarasa ya Qur'ani na kuniunga mkono kila hatua," alifafanua.
Ridhai anaamini kwamba kufuata mafundisho ya Qur’ani ndio ufunguo wa furaha ya kweli. "Qur'an siku zote ni chanzo cha mwongozo. Mtu akiizingatia hata kwa kiwango cha chini, atavutiwa sana na uzuri wake kiasi kwamba hawezi kuvumilia kutenganishwa nayo," alisema.
Akihutubia wale wanaotaka kuhifadhi Qur’ani kwa ukamilifu, aliwahimiza kuendelea na jitihada hiyo. "Kadiri mtu anavyojishughulisha zaidi na njia hii, ndivyo watakavyoonja utamu wake zaidi. Kiu ya kupendeza ya kujifunza Qur’ani itawashika," aliongeza.
Sasa Bi.Ridhai ambaye ni mwalimu katika kijiji cha mashambani anaridhika katika kufundisha. Anasisitiza umuhimu wa kujenga imani kwa wanafunzi wake ili kuwatia moyo kuelekea atika njia ya kuikumbatia Qur’ani.
Kwa walimu wanaolenga kuwaongoza wanafunzi kuelekea atika kujifunza Qur’ani, Bi. Ridhai anatetea kurekebisha mtazamo wao kwa mtazamo wa watoto. "Mwalimu, haswa ambaye ni msomaji au mwenye kuhifadhi Qur'ani, lazima awasilishe kiini cha Qur’ani kwa njia inayowavutia wasikilizaji wao. Unapaswa kuzungumza kwa lugha ya mtoto wa miaka saba na kuzingatia historia yake wakati wa kuwasilisha dhana yoyote ," alisema.
Bi. Ridhai aliangazia thamani ya mbinu za kufundisha zisizo za moja kwa moja, akipata msukumo kutoka kwa mila za Kiislamu. "Kama vile Imam Hassan (AS) na Imam Hussein (AS) walivyomfundisha mzee jinsi ya kutawadha kwa njia ya mwongozo usio wa moja kwa moja, mtu yeyote anayejishughulisha na elimu ya kitamaduni leo lazima ajue mbinu ya mafundisho yasiyo ya moja kwa moja," alishauri.
Alipoulizwa kuhusu aya ya Qur’ani inayomletea amani zaidi, Bi. Ridhai alinukuu aya ya 17 kutoka kwenye Surah As-Sajdah: “Nafsi yoyote haijui waliyo fichiwa (Akhera) katika hayo yanayo furahisha macho - ni malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda.. ”
"Ayah hii inanigusa sana," alisema.
4252629