IQNA

Mashindano ya Kitaifa ya Qur'ani

Waliofika fainali ya mashindano ya 47 ya Kitaifa ya Qur'ani ya Iran watangazwa

14:54 - November 18, 2024
Habari ID: 3479772
IQNA - Jumuiya ya Masuala ya Wakfu na Misaada Iran imetangaza waliofuzu katika Mashindano ya 47 ya Kitaifa ya Qur'ani nchini Iran.

Washindi wa fainali za mwaka huu ni pamoja na washiriki kutoka kategoria za wanaume na wanawake, pamoja na washindani walio chini ya umri wa miaka 18, katika taaluma mbalimbali kama vile kuhifadhi, qiraa, kusoma dua, na adhana.

Jumla ya washiriki 225 wamefanikiwa kutinga hatua ya fainali ya mashindano hayo ya kitaifa yatakalofanyika kuanzia tarehe 2 Desemba hadi Disemba 19 huko Tabriz, Mkoa wa Azarbaijan Mashariki.

Tukio hilo litaashiria kilele cha tukio kuu la Qur'ani la Iran, lenye lengo la kukuza vipaji vya Qur'ani na kuhimiza ushirikiano wa kina na Qur'ani Tukufu katika jamii.

Mashindano hayo yaliyoanza mwanzoni mwa mwaka huu yalishirikisha hatua mbalimbali zikiwemo za awali, mikoa na kitaifa.

Ingawa hatua za awali zilijumuisha mawasilisho ya ana kwa ana na ya video kwa ajili ya kuhukumu, hatua ya mwisho itawaleta maqari wakuu wa taifa na wakariri pamoja kwa ajili ya shindano la ana kwa ana.

Mashindano ya mwaka huu ya kauli mbiu ya  "Mashahidi wa Huduma," ikiwa ni pamoja na Rais wa zamani Ebrahim Raisi na wenzake, ambao walifufa shahidi katika ajali ya helikopta mwezi Mei.

Washindi wa mashindano hayo wataiwakilisha Iran katika matukio ya kimataifa ya Qur'ani kote duniani.

3490729

Habari zinazohusiana
captcha