IQNA

Mashindano ya Qur'ani

Fainali za Mashindano ya Kitaifa ya Quran ya Iran

20:40 - December 03, 2024
Habari ID: 3479849
IQNA - Mji wa kaskazini-magharibi wa Tabriz ni mwenyeji wa hatua ya mwisho ya Mashindano ya 47 ya Kitaifa ya Qur'ani ya Iran, yaliyoanza kwa sherehe Jumatatu asubuhi.

Sherehe hiyo ilianza kwa usomaji wa aya za Qur'ani Tukufu na qari mashuhuri Saeed Parvizi, na kisha Hujjatul Islam Seyed Shahabeddin Hosseini, mkurugenzi mkuu wa Idara ya Wakfu ya Mkoa wa Azarbaijan Mashariki, alihutubia hadhirina.

Ametoa salamu za rambirambi kwa mnasaba wa kumbukumbu ya kuuawa shahidi Bibi FatimaHazrat Zahra (SA) na kueleza kuandaa mashindano ya Qur'ani kuwa ni chanzo cha heshima kwa mji huo ambao umewahi kuwa makao ya wanazuoni kadhaa za Kiislamu wa ngazi za juu wa ulimwengu wa Shia akiwemo mfasiri wa Qur'ani Allamah Seyed Mohammad Hossein. Tabatabai.

Hujjatul Islam Ahmad Motahariasl, mwakilishi wa Kiongozi Muadhamu wa wa Mapinduzi ya Kiislamu katika jimbo hilo pia amehutubia katika hafla hiyo akiashiria malipo ya Mwenyezi Mungu kwa vijana wanaosoma Qur'ani.

Vile vile alisisitiza jinsi ilivyo muhimu kwa wazazi kuwafundisha watoto wao Qur'ani na kuwahimiza wampenda Mtume Muhammad (SAW) na Ahl-ul-Bayt wake (AS).

Mashindano hayo yaliyoanza mwanzoni mwa mwaka huu, yamekuwa hatua mbalimbali zikiwemo za awali, mikoa na kitaifa.

Jumla ya washiriki 225 wamefuzu kwa hatua ya fainali itakayoendelea hadi Desemba 19 huko Tabriz.

Tukio la mwaka huu linafanyika kwa kauli mbiu ya "Mashahidi wa Huduma," ikiwa ni pamoja na Rais wa zamani Ebrahim Raisi na wenzake, ambao walipoteza maisha yao katika ajali ya helikopta mwezi Mei.

Washindi wa mashindano hayo wataiwakilisha Iran katika matukio ya kimataifa ya Qur'ani kote duniani.

3490911

Habari zinazohusiana
captcha