IQNA

Waandishi habari wa Italia wapongeza huduma katika Haram ya Imam Hussein (AS)

16:26 - May 02, 2025
Habari ID: 3480622
IQNA – Ujumbe wa ngazi ya juu wa vyombo vya habari kutoka Italia, uliotembelea taasisi kadhaa chini ya Idara ya Mfawidhi wa Haram Takatifu ya Imam Hussein (AS), huko Karbala, Iraq umesifu huduma za kisasa zinazotolewa na idara hiyo katika nyanja mbalimbali, hasa afya na elimu.

Ujumbe huo ulitembelea taasisi hizo katika mfumo wa mipango iliyoandaliwa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Iraq na Idara ya Utalii ya nchi hiyo, kwa ushirikiano na Kituo cha Kimataifa cha Habari cha Idara ya Mfawidhi wa Haram Takatifu ya Imam Hussein (AS).

Moja ya vituo vilivyotembelewa na wanahabari hao wa Italia ni Kituo cha Imamu Hadi (AS), kilicho chini ya Kitengo cha Afya na Elimu ya Tiba cha Idara ya Mfawidhi wa Haram Takatifu ya Imam Hussein (AS

Walizunguka sehemu mbalimbali za kituo hicho na kufahamu asili ya kazi zake pamoja na teknolojia za kisasa za matibabu zinazotumika hapo.

Pia walitembelea Chuo Kikuu cha Al-Zahra kwa wasichana huko Karbala na wakajifunza kuhusu shughuli na programu zake za kitaaluma na kielimu.

Ujumbe huo wa vyombo vya habari pia ulitembelea maeneo kadhaa ya kidini na ya utalii nchini Iraq, ukiweka mkazo kwenye kuanzisha shughuli za kitamaduni na masuala ya kiakili yanayohusiana na dini, kupambana na misimamo mikali na itikadi kali, kukuza utamaduni wa kuishi pamoja kwa amani, na kupinga aina mbalimbali za ubaguzi wa rangi.

3492900

captcha