IQNA

Maandamano yafanyika Asia Magharibi kuunga mkono Iran

14:58 - June 21, 2025
Habari ID: 3480849
IQNA-Maandamano yamefanyika katika nchi kadhaa za eneo siku ya Ijumaa kutangaza kufungamana na Iran wakati huu wa kukabiliana na hujuma ya kichokozi na kijinai ya utawala wa Kizayuni wa Israel.

Nchini Yemen maandamano makubwa yamefanyika katika mikoa wa Saada ambapo wananchi wametoa nara za kulaani hujuma ya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na pia jinai ya mauaji ya kimbari ya utawala huo dhidi ya Gaza.

Katika miji ya Baghdad, Karbala, na Kufa nchini Iraq, maelfu wamejitokeza mitaani  kuutaja utawala haramu wa Israel na Marekani kuwa maadu wakuu wa mataifa ya Waislamu.

Wamesema utawala wa Kizayuni wa Israel umekiuka maadili yote ya kibinadamu kwa kushambulia mahospitali, vituo vya kielimu na maeneo mengine ya raia nchini Iran. Waandamanaji waliokuwa na hasira pia wameteketeza moto bendera za utawala haramu wa Israel.

Maandamano sawa na hayo yamefanyika Pakistan katika miji ya Islamabad, Lahore na Karachi.

Regional Countries Host Rallies in Solidarity with Iran

Huku wakiwa wanapeperusha bendera za Pakistan na Iran, waandamanaji walitoa nara dhidi ya Israel na Marekani sambamba na kutangaza kufungamana na operesheni za kijeshi za Iran dhidi ya Israel.

Nchini Lebanon pia kumefanyika maandamano katika mji mkuu, Beirut kulaani jinai za Israel dhidi ya Iran na Gaza.

Halikadhalika wanazuoni wa Kiislamu wa Lebanon na Palestina wamekutana huko Tyre, Lebanon na kulaani uchokozi wa Israel dhidi ya Iran. Aidha wamelaani vikali vitisho vya Rais  Donald Trump wa Marekani dhidi ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei.

Regional Countries Host Rallies in Solidarity with Iran

Wazungumzaji katika kikao hicho wamesema Iran inakabiliana na ugaidi wa Marekani na utawala wa Kizayuni na kuongeza kuwa huu ni ugaidi usiotambua maadili ya ubinadamu, kinga ya vyombo vya habari na hukiuka kiholela  sheria na kanuni za kimataifa. Wanazuoni hao wa Kiislamu wa Palestina na Lebanon wametoa wito kwa Waislamu duniani kote kusimama dhidi ya mradi wa Marekani na utawala wa Kizayuni ambao unaelnga kuangamiza Palestina, Lebanon, Iran, Syria, Iraq na Yemen.

3493516

Habari zinazohusiana
Kishikizo: iran vita israel
captcha