“Zayuni mwenye misimamo mikali yakdini kutoka kundi lenye mwelekeo wa Wanazi mamboleo amechoma Qur’ani Tukufu hadharani, bila kuficha uso wake,” alisema mbunge wa Kiarabu katika Bunge la Israel (Knesset), Ahmad Tibi, kupitia mtandao wa kijamii wa X .
Tibi amelalamika kuwa mlowezi huyo mwenye misimamo mikali “hataadhibiwa kwa sababu yeye ni Myahudi.”
Katika video aliyoshiriki Tibi, mlowezi huyo haramu wa Kizayuni anasikika akisema: “Kuna nini kinaendelea? Tuko hapa sasa tunasherehekea na kuchoma kitabu kitakatifu sana kwa Waislamu, sura kwa sura, sura zote. Hongera kwetu.”
Aliendelea kusema: “Watu wa Israel wanaondoa uovu. Hongera kwetu. Ninaiheshimu sana Qur’ani, lakini pale inapokuwa katika hali hii,” huku akiendelea kuchoma Kitabu Kitakatifu.
Hakukuwa na kauli ya haraka kutoka kwa utawala wa Kizayuni wa Israel wala kutoka kwa makundi ya Kiyahudi kuhusu tukio hilo, wakati huu Waislamu duniani kote wakianza kuukaribisha na kuadhimisha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
3496456