IQNA

Kundi la Waislamu Kanada Lapya Wito wa Mkakati wa Kukabiliana na Chuki Dhidi ya Uislamu

22:17 - June 05, 2026
Habari ID: 3482323
IQNA – Miaka mitano baada ya mwanaume mmoja kuendesha kwa makusudi gari aina ya pickup na kuigonga familia ya Kiislamu iliyokuwa ikitembea kwa miguu mjini London, katika jimbo la Ontario, Kanada, na kuwaua watu wanne, kundi la kitaifa la utetezi wa haki za Waislamu limesema kuwa serikali ya shirikisho imeshindwa kutekeleza mapendekezo muhimu ya kukabiliana na chuki dhidi ya Uislamu.

Siku ya Jumamosi itaadhimisha kumbukumbu ya kuuawa kwa familia ya Afzaal katika shambulio hilo mjini London, Ontario.

Mshambuliaji huyo alipatikana na hatia ya makosa manne ya mauaji na kosa moja la jaribio la mauaji, baada ya kuendesha gari lake na kuligonga familia iliyokuwa imevalia mavazi ya jadi ya Kiislamu.

Baraza la Masuala ya Umma la Waislamu wa Kanada (Canadian Muslim Public Affairs Council) linaadhimisha tukio hilo kwa kuchapisha ripoti mpya inayoiomba serikali ya Ottawa kuongeza juhudi katika kupambana na chuki dhidi ya Waislamu.

Kundi hilo pia linataka kutengwa kwa dola milioni 40 za ufadhili wa serikali ya shirikisho kwa ajili ya kulinda misikiti na shule za Kiislamu, likisema kuwa kiwango hicho ni sawia na fedha zilizotengwa hivi karibuni kwa taasisi za Kiyahudi.

Takwimu za Shirika la Takwimu la Kanada (Statistics Canada) zinaonesha kuwa taarifa za jumla za uhalifu wa chuki nchini humo karibu zimeongezeka mara tatu kati ya mwaka 2018 na 2024, hali iliyochangiwa kwa kiasi kikubwa na ongezeko la chuki dhidi ya Uislamu na pia chuki dhidi ya Wayahudi.

Ripoti hii ya The Canadian Press ilichapishwa kwa mara ya kwanza tarehe 4 Juni 2026.

3497719

Habari zinazohusiana
captcha