IQNA

Mahujaji Wapokea Nakala Milioni 1.9 za Qur’ani wakati wa kuondoka Saudia

13:26 - June 02, 2026
Habari ID: 3482314
IQNA – Wakiwa na mizigo mikononi mwao lakini nyoyo zao zikiwa bado zimejaa athari za ibada za Hija, mahujaji waliokuwa wakiondoka walikabidhiwa kila mmoja zawadi yanakala ya Qur’ani Tukufu.

Jumla ya nakala milioni 1.9 za Qur’ani Tukufu pamoja na tafsiri za maana zake zilisambazwa kwa mahujaji waliokuwa wakiondoka kupitia vituo vya usafiri wa anga, nchi kavu, na baharini, pamoja na watumishi walioshiriki katika msimu wa Hajj wa mwaka 1447 Hijria, ikiwa ni sehemu ya programu na huduma zilizotolewa sambamba na Hajj.

Zawadi hiyo ilijumuisha nakala za Qur’ani Tukufu na tafsiri za maana zake zilizochapishwa na Taasisi ya Mfalme Fahd ya Uchapaji wa Qur’ani Tukufu ilioko Madina, na kutafsiriwa katika lugha 80 za dunia, jambo lililowezesha wahujaji kunufaika na maana za Qur’ani katika lugha zao za asili.

Taasisi hiyo inaendelea kuchapisha nakala za Qur’ani na tafsiri za maana zake katika lugha nyingi za kimataifa kwa kuzingatia viwango madhubuti vya uchapaji, uhakiki, na tafsiri. Juhudi hizi zinachangia kupanua upatikanaji wa maudhui ya Qur’ani miongoni mwa Waislamu duniani kote.

Usambazaji wa nakala hizi unakuja kama sehemu ya programu na huduma zinazotolewa katika msimu wa Hija, kwa lengo la kuimarisha tajriba ya kidini na kielimu ya wahujaji baada ya kukamilisha ibada zao.

3497684

captcha