arbaeen - Ukurasa 4

IQNA

Arbaeen 1446
IQNA - Mawkib yenye jina la "Neda al-Aqsa" (Wito wa Al Aqsa) imeundwa kwenye nguzo nambari 833 ya barabara ya Najaf-Karbala nchini Iraq katika matembezi ya Arbaeen ya mwaka huu. Mawkiba hii inakaribisha wafanyaziara na maafisa ambao husimama ili kutoa sauti zao za mshikamano. na Wapalestina huku kukiwa na mauaji ya kimbari ya Israel huko Gaza.
Habari ID: 3479315   Tarehe ya kuchapishwa : 2024/08/23

Arbaeen 1446
IQNA - Wajumbe wa msafara wa Qur'ani wa Iran hadi sasa wameandaa programu 650 tofauti kwa wafanyaziara wa Arbaeen nchini Iraq.
Habari ID: 3479313   Tarehe ya kuchapishwa : 2024/08/23

Arbaeen na Muqawama
IQNA - Kundi la wasomaji Qur’ani (maqari) wa Kiirani walioenda Iraq wakati wa msimu huu wa Arbaeen wameshiriki katika vikao vya  kusoma Qur'ani kwenye kaburi la Shahidi Abu Mahdi al-Muhandis, naibu mkuu wa zamani wa VJeshi la Kujitolea la Wananchi wa Iraq (PMU).
Habari ID: 3479310   Tarehe ya kuchapishwa : 2024/08/21

Arbaeen 1446
IQNA - Huku mamilioni ya wafanyaziara au mazuwar wakiwa wanashiriki katika matembezi ya Arbaeen, wataalamu wanasisitiza umuhimu wa kudumisha mlo sahihi ili kuhakikisha afya na ustawi njiani.
Habari ID: 3479308   Tarehe ya kuchapishwa : 2024/08/21

Arbaeen 1446
IQNA - Kundi la wanaharakati wa Qur'ani wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Al-Mustafa wamelekea Iraq Jumatatu jioni kushiriki katika matembezi ya Arbaeen ya Imam Hussein (AS).
Habari ID: 3479305   Tarehe ya kuchapishwa : 2024/08/20

Arbaeen
IQNA – Assad Al Eidani Gavana wa Basra kusini mwa Iraq ametangaza siku tatu za likizo ya umma katika mkoa huo kwa munasaba wa  Arbaeen ya Imam Hussein (AS)
Habari ID: 3479304   Tarehe ya kuchapishwa : 2024/08/20

Arbaeen katika Qur'an /3
IQNA – Wakati Arbaeen, maana yake ni arobaini na arubaini, ni neno linalohusiana na wingi, katika maandiko mengi ya Kiislamu na Hadithi, linatumika kurejelea sifa na ukuaji wa kiroho wa mwanadamu.
Habari ID: 3479302   Tarehe ya kuchapishwa : 2024/08/19

Arbaeen 1446
IQNA – Jumba la Makumbusho la Al-Kafeel, lenye mafungamano na Haram Takatifu ya Hazrat Abbas (AS), limeweka Mawkib kwenye barabara ya Najaf-Karbala ili kuwahudumia wafanyaziara wa Arbaeen.
Habari ID: 3479301   Tarehe ya kuchapishwa : 2024/08/19

IQNA - Wanachama wa kike wa Msafara wa Qur'ani wa Arbaeen wa Iran, unaojulikana kama Msafara wa Noor, wameanza kuandaa programu za Qur'ani kwa ajili ya mazuwar.
Habari ID: 3479300   Tarehe ya kuchapishwa : 2024/08/19

Arbaeen 1446
IQNA - Mawkib kwa ajili ya wafanyaziara au mazuwar wa Arbaeen wanaozungumza Kiingereza itazinduliwa Karbala, Iraq, katika siku zijazo.
Habari ID: 3479298   Tarehe ya kuchapishwa : 2024/08/19

Arbaeen 1446
IQNA - Mkurugenzi wa Taasisi ya Qur'ani inayohusishwa na Haram ya Hazrat Abbas (AS) huko Karbala ametangaza kuanza kwa programu maalum za Qur'ani kwa wafanyaziara wa Arbaeen.
Habari ID: 3479296   Tarehe ya kuchapishwa : 2024/08/18

Arbaeen 1446
IQNA - Waziri Mkuu wa Iraq alisema idadi ya wafanyaziara wa Arbaeen kutoka Iraq na nje ya nchi inatarajiwa kufikia milioni 23 mwaka huu.
Habari ID: 3479294   Tarehe ya kuchapishwa : 2024/08/18

Arbaeen katika Qur’ani /2
IQNA – Neno Arbaeen (maana ya siku arubaini) limetajwa ndani ya Qur’ani Tukufu kuhusu Miqat ya Musa (AS) na kuhusu jinsi Bani Isra’il walivyokwama. Kuna aya 4 ndani ya Qur’ani Tukufu ambamo Arbaeen imetajwa, 3 kati yake ni kuhusu Bani Isra’il.
Habari ID: 3479292   Tarehe ya kuchapishwa : 2024/08/18

Arbaeen 1446
IQNA - Makamu wa Kwanza wa Rais wa Iran Mohammad Reza Aref amesisitiza haja ya kutoa huduma bora kwa wafanyaziara wa Arbaeen.
Habari ID: 3479287   Tarehe ya kuchapishwa : 2024/08/16

Arbaeen katika Qur'an/1
IQNA – Kuna idadi au nambari 39 zilizotajwa ndani ya Qur'an, baadhi yake zinarejelea tu nambari, wakati zingine zina siri nyuma yake.
Habari ID: 3479282   Tarehe ya kuchapishwa : 2024/08/15

Arbaeen 1446
IQNA - Makao Makuu makuu ya Iran ya Arbaeen yanasema idadi ya wafanyaziara wa Iran wanaosafiri kwenda Iraq kwa ajili ya kushiriki matembezi ya mwaka huu ya Arbaeen hadi sasa ni zaidi ya 650,000.
Habari ID: 3479279   Tarehe ya kuchapishwa : 2024/08/14

Kadhia ya Palestina
IQNA - Washiriki katika mkutano wa kimataifa huko Karbala, Iraq wamesisitiza haja ya mshikamano na watu wa Palestina na kususia utawala wa Kizayuni wa Israel.
Habari ID: 3479278   Tarehe ya kuchapishwa : 2024/08/14

IQNA - Watu kutoka Ra's al-Bisha, wilaya ya kusini mwa Iraq, walianza safari yao ya miguu hadi Karbala kuashiria Arbaeen mapema Agosti 2024. Waumini hao wanatazamiwa kutumbea masafa ya kilomita 615 kuonyesha mapenzi yao kwa Imam Hussein (AS)
Habari ID: 3479276   Tarehe ya kuchapishwa : 2024/08/13

Arbaeen 1446
IQNA - Wanachama wa msafara wa Qur'ani wa Arbaeen wa Iran wametajwa na kundi hilo linajumuisha wasomaji Qur'ani waalikwa kutoka nchi 14.
Habari ID: 3479275   Tarehe ya kuchapishwa : 2024/08/13

Arbaeen 1446
IQNA - Kituo cha Dar-ul-Quran chenye mfungamano na Mfawidhi wa Kaburi Takatifu la Imam Ali (AS) kitaendesha programu za Qur'ani kwa wafanyaziara wakati wa matembezi ya Arbaeen mwaka huu.
Habari ID: 3479269   Tarehe ya kuchapishwa : 2024/08/12