iqna

IQNA

TEHRAN (IQNA)- Waislamu zaidi ya milioni mbili walifurika katika Msikiti Mkuu wa Makka (al-Masjid al-Haram) na Msikiti wa Mtume SAW (al-Masjid an-Nabawi) mjini Madina Jumatatu.
Habari ID: 3471556    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/06/13

TEHRAN (IQNA)-Serikali ya Saudi Arabia imewapiga marufuku mahujaji na wafanyaziara kupiga picha au kuchukua video kwa kutumia chombo chochote katika Misikiti Miwili Mitakatifu ya Kiislamu ya Makka na Madina.
Habari ID: 3471279    Tarehe ya kuchapishwa : 2017/11/25

TEHRAN (IQNA)-Mahakama moja nchini Saudi Arabia imesema Shirika la Ujenzi la Binladin halina hatia na haliwezi kubebeshwa dhima ya kuanguka winchi (crane) katika Msikiti Mtakatifu wa Makka wakati wa msimu wa Hija mwaka 2015.
Habari ID: 3471203    Tarehe ya kuchapishwa : 2017/10/03

TEHRAN (IQNA)-Kongamano la Kimataifa la Hija linafanyika Agosti 26-27 katika mji takatifu wa Makka ambapo wanazuoni wa Kiislamu kutoka mabara yote duniani wanashiriki.
Habari ID: 3471143    Tarehe ya kuchapishwa : 2017/08/26

TEHRAN (IQNA)- Utawala wa Kizayuni wa Israel sasa utatimiza ndoto yake ya muda mrefu ya kuuteka mji mtakatifu wa Makka kupitia msaada wa Muhammad bin Salman, mrithi mpya wa kiti cha ufalme nchini humo.
Habari ID: 3471048    Tarehe ya kuchapishwa : 2017/07/03

IQNA-Gazeti moja mashuhuri nchini Brunei limefungwa baada ya kuandika kuwa matatizo ya kiuchumi Saudi Arabia yameipelekea iongeze kwa kiasi kikubwa bei ya Visa ya Hija.
Habari ID: 3470664    Tarehe ya kuchapishwa : 2016/11/09

Abdulswamad bin Omar Muhammad kutoka Somalia ndie mshiriki mwenye umri mdogo zaidi katika mashindano ya kimataifa ya Qur'ani Tukufu Saudi Arabia.
Habari ID: 3446375    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/11/09

Umoja wa Wanawake Waislamu Duniani wametoa taarifa ya rambirambi kufuatia kuuawa maelfu ya mahujaji kutoka nchi mbali mbali katika mkanyangano wa Mina karibu na mji mtakatifu wa Makka.
Habari ID: 3385195    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/10/13

Tarehe 24 Septemba katika siku kuu ya Idul Adha wakati zilipoenea habari za kukanyagana na kuzimia baadhi ya Mahujaji huko Mina, hakuna aliyedhani au kuamini kuwa tukio hilo lingegeuka na kuwa maafa makubwa na ya kuogofya ambayo yameshuhudiwa.
Habari ID: 3381643    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/10/05

Serikali ya Indonesia imesema siku kadhaa baada ya maafa ya Mina, utawala wa Saudi Arabia umeizuia nchi yake kuwatambua au kutoa msaada wa kitiba kwa raia wake.
Habari ID: 3375825    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/09/30

Sayyid Hassan Nasrullah
Katibu Mkuu wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa Saudi Arabia inalazimika kukabidhi masuala ya kusimamia na kuendesha ibada ya Hija kwa nchi za Kiislamu.
Habari ID: 3370688    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/09/26

Idara ya Mfalme wa Saudi Arabia, Salman bin Abdul Aziz imelizuia shirika la ujenzi la Bin Ladin kuendelea na shughuli zake za ujenzi nchini humo baada ya kutokea ajali ya kreni auwinchi iliyopelekea zaidi ya mahujaji 107 kufariki dunia mjini Makka.
Habari ID: 3363334    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/09/16

Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu amesema uzembe uliofanywa na serikali ya Saudi Arabia ndio uliosababisha tukio la maafa yaliyotokea katika mji mtukufu wa Makka.
Habari ID: 3362440    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/09/14

Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametuma salamu za rambi rambi kufuatia ajali ya kusikitisha katika mji Mtakatifu wa Makka siku ya Ijumaa.
Habari ID: 3361981    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/09/13

Wafanyaziara wasiopungua 107 wamefariki dunia baada ya kuangukiwa na kreni au winchi katika Msikiti Mtakatifu wa Makka, Saudi Arabia.
Habari ID: 3361271    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/09/11

Gazeti moja la Uingereza hivi karibuni limechapisha orodha ya misikiti 25 bora duniani kwa mtazamo wa usanifu majengo.
Habari ID: 3338961    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/08/04

Duru ya 36 ya Mashindano ya Kimatiafa ya Hifdhi, Qiraa na Tafsiri ya Qur’ani Tukufu yameanza leo Novemba 15 katika Msikitu Mkuu wa Makka (Masjid al-Haram) , Saudi Arabia.
Habari ID: 1473482    Tarehe ya kuchapishwa : 2014/11/15

Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wa Bangladesh Abdul Latif Siddique amefukuzwa kazi kwa kuvunjia heshima ibada ya Hija na Mtume Muhammad (saw).
Habari ID: 1456641    Tarehe ya kuchapishwa : 2014/10/03