IQNA

Turathi

Urekebishaji wa Nakala Adimu ya Msahafu wa Karne ya 10 Kuanza Karbala

22:42 - January 17, 2025
Habari ID: 3480063
IQNA – Urekebishaji wa kurasa za nakala adimu ya Msahafu (Qur'ani) wa karne ya 10 Miladia umeanza huko Karbala, Iraq. Haya ni kwa mujibu wa Latif Abdulzahra, mkuu wa Idara ya Urekebishaji Nakala katika Kituo cha Kuhifadhi Nakala na Kumbukumbu katika kaburi au Haram ya Hazrat Abbas (AS).

"Kama sehemu ya mpango wa mwaka 2025, kituo kimeanza kurekebisha nakala adimu ya Qur'ani kutoka karne ya 10, ambayo inahifadhiwa katika maktaba ya Haram ya Abbasi," alisema.

Alifafanua kuwa mchakato wa urekebishaji unahusisha hatua kadhaa, ikiwemo uchunguzi wa kibaiolojia na kemikali, kurekebisha kurasa, na kutengeneza sanduku maalum kwa ajili ya kuhifadhi kabla ya kuirejesha kwenye eneo la kuhifadhiwa ndani ya Haram.

Abdulzahra alielezea awamu ya awali ya urekebishaji, ambao unajumuisha uchunguzi wa kina wa nakala hiyo, karatasi zake, rangi, mapambo, na wino uliotumika kuandika.

3491484

"Tunapiga picha uharibifu na kuweka nambari za kurasa kulingana na mpangilio wa Qur'ani kabla ya kuanza urekebishaji wowote," aliongeza.

Alibainisha kuwa nakala hiyo imeharibiwa kutokana na mazingira na uhifadhi usiofaa, na kusababisha kurasa kuharibika na sehemu kuachana.

Lengo la kurekebisha Misahafu kama hii ni kuhifadhi na kuilinda dhidi ya hali ya mazingira ya baadaye, aliongeza.

Habari zinazohusiana
Kishikizo: msahafu kale
captcha