iqna

IQNA

IQNA-Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina , Hamas, imelinganisha vitendo vya utawala haramu wa Israel katika Ukanda wa Gaza na mauaji ya kimbari ya Rwanda, huku ikisifu hatua ya Umoja wa Afrika Afrika kumfukuza balozi wa utawala wa Israel kutoka mkutano maalum wa kumbukumbu uliofanyika Addis Ababa, Ethiopia.
Habari ID: 3480514    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/04/08

IQNA-Mufti Mkuu wa Oman, Sheikh Ahmed al-Khalili, amekosoa vikali kimya kinachoonyeshwa mbele ya jinai za kinyama zinazofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3480497    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/04/05

IQNA – Mashambulizi ya anga ya utawala katili wa Israel katika Ukanda wa Gaza unaozingirwa yamesababisha vifo vya zaidi ya watu 100, wakiwemo 33 waliokuwa wakijisitiri katika shule.
Habari ID: 3480492    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/04/04

IQNA – Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) limeripoti kuwa zaidi ya watoto 300 wameuawa Gaza tangu vikosi vya utawala wa Kizayuni wa Israel vilipoanza upya vita mnamo Machi 18.  
Habari ID: 3480484    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/04/02

IQNA- Swala ya Ijumaa ya mwisho wa mwezi mtukufu wa Ramadhani katika misikiti mbalimbali duniani, ikiwemo Msikiti wa Masjid al Al-Haram katika mji mtakatifu wa Makka, na Msikiti wa Al-Azhar nchini, iliandamana na dua kwa ajili ya Wapalestina wa Gaza na Msikiti wa Al-Aqsa.
Habari ID: 3480464    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/03/29

IQNA – Jiji la Vienna, mji mkuu wa Austria, lilishuhudia maandamano makubwa yanayopinga kuendelea kwa mashambulizi ya Israel dhidi ya Gaza. Waandamanaji walibeba mabango na vipeperushi vyenye maandiko, “Acha kuua watoto,” “Acha vita sasa,” na “Susia Israel."
Habari ID: 3480427    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/03/24

IQNA-Vikosi vya Jeshi la Yemeni vimetan gaza shambulio jingine dhidi ya vikosi vya Marekani katika eneo la Bahari ya Shamu, vikitumia makombora na ndege zisizo na rubani ili kuzuia shambulio tarajiwa la Marekani dhidi ya nchi hiyo ya Kiarabu.
Habari ID: 3480393    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/03/18

IQNA – Harakati ya Ansarullah ya Yemen imeahidi kujibu uchokozi wa kijeshi wa hivi karibuni wa Marekani, kufuatia mashambulizi ya angani ya Marekani na Uingereza ambayo yalilenga maeneo kadhaa kote nchini, ikiwemo mji mkuu, Sanaa, na jimbo la kaskazini la Saada.
Habari ID: 3480380    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/03/16

IQNA-Mufti Mkuu wa Oman amewataka Waislamu wote na watu wanaopenda uhuru duniani kusaidia watu wanaodhulumiwa wa Gaza wanaoishi katika hali mbaya.
Habari ID: 3480336    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/03/09

IQNA-Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) imetoa taarifa rasmi mwishoni mwa kikao chake cha mjini Jeddah, Saudi Arabia na kulaani kwa nguvu zote njama za Marekani na Israel za kutaka kuwahamisha kwa nguvu Wapalestina wa Ukanda wa Ghaza.
Habari ID: 3480334    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/03/09

IQNA – Wakati ulimwengu wa Kiislamu ukikaribisha mwezi mtukufu wa Ramadhani, Katibu Mkuu wa Shirika la Ushirikiano wa Kiislamu (OIC), Hissein Brahim Taha, amemuomba Mwenyezi Mungu aujali mwezi huu uwe "hatua muhimu” katika ukombozi wa ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu.
Habari ID: 3480284    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/03/01

IQNA-Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, akiwapongeza wapiganaji wa Muqawama kwa ushindi wao katika Ukanda wa Gaza, amesisitiza kwamba kazi kubwa ya viongozi na wapiganaji wa Muqawama wa Palestina ipo katika "umoja na mshikamano" na "kusimama imara" dhidi ya adui, kuendesha mchakato mgumu wa mazungumzo, pamoja na uvumilivu na ustahimilivu wa wananchi, ambavyo vimeinua heshima ya Muqawama katika eneo.
Habari ID: 3480233    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/02/18

IQNA-Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon Sheikh Naeem Qassim, amesema katika hotuba aliyotoa kwa mnasaba wa kumbukumbu ya kuwaenzi makamanda waliouawa shahidi kwamba: Haj Imad Mughniyah alikuwa shakhsia wa kiusalama na kijeshi na mbunifu ambaye aliwaongoza Mujahidina kwa msingi wa moyo wa imani.
Habari ID: 3480230    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/02/17

IQNA – Mchambuzi wa kisiasa wa Iraq alisema vita vya Gaza vilikuwa sehemu ya njama ya Marekani-Uzayuni za kuangamiza harakati za Muqawama au mapambano ya Kiislamu katika eneo la Asia Magharibi. Akizungumza katika mahojiano na IQNA kuhusu hali ya Gaza na usitishaji mapigano kati ya Hamas na utawala wa Israel, Sannan al-Saadi amesema Rais wa Marekani Donald Trump sasa anatafuta kukamilisha mradi huu.
Habari ID: 3480225    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/02/16

Kadhia ya Palestina
IQNA-Makumi ya maelfu ya wananchi wa Morocco wamejitokeza katika kona zote za nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika kushiriki maandamano ya kuunga mkono kadhia ya Palestina na kupinga mpango wa Rais Donald Trump wa Marekani kuhusu Gaza.
Habari ID: 3480221    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/02/15

IQNA-Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imetoa wito kwa Wapalestina, Waarabu, Waislamu na watu huru kote duniani kushiriki katika harakati ya kimataifa siku za Ijumaa, Jumamosi na Jumapili, ili kupinga mipango ya Rais Donald Trump wa Marekani ya kuwaondoa Wapalestina katika Ukanda wa Gaza na kulikalia kwa mabavu eneo hilo.
Habari ID: 3480219    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/02/14

IQNA-Harakati ya Mpambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imekariri upinzani wake dhidi ya matamshi yaliyotolewa Rais Donald Trump wa Marekani kuhusu suala la kuwahamusha makazi Wapalestina kutoka Ukanda wa Gaza kwa kisingizio cha kulijenga upya eneo hilo.
Habari ID: 3480213    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/02/13

Jinai za Israel
IQNA – Mwaka jana ulikuwa mwaka wa vifo vingi zaidi katika historia ya waandishi wa habari, ambapo vifo 124 viliripotiwa, ambapo utawala wa Israeli unahusika na asilimia 70 ya vifo hivyo. Hii ni kulingana na Tume ya Kulinda Waandishi wa Habari (CPJ).
Habari ID: 3480209    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/02/13

Kadhia ya Palestina
Trump kupoteza dau lake kuhusu Gaza, asema mchambuzi IQNA – Mchambuzi kutoka Tunisia anasema kwamba Rais wa Marekani Donald Trump atashindwa katika dau lake kuhusu Gaza kwani mpango wake wa kuwafurusha Wapalestina kutoka eneo lililozungukwa umepokelewa kwa upinzani mkubwa.
Habari ID: 3480202    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/02/12

IQNA - Safari ya leo ni katika mkutano na Rais wa Baraza la Utawala la Hamas, Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei,  ambapo aliheshimu mashahidi wa Gaza pamoja na makamanda wa mashahidi, hasa shahidi Isma'il Haniyyah, akizungumza na viongozi wa Hamas na kusema: 'Mmefanikiwa kuondoa serikali ya Wazayuni, na kwa kweli, kwa ridhaa ya  Mwenyezi Mungu, Marekani haikuruhusu kutimiza malengo yao. 
Habari ID: 3480183    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/02/09