Akizungumza katika hafla ya ufunguzi wa shindano hilo katika Eneo la Serikali ya Mtaa ya Jama’are jimboni humo, Gavana wa Jimbo la Bauchi Bala Mohammed alifichua serikali imechangia Naira milioni 130 kwa ajili ya kuandaa shindano hilo.
Gavana huyo alibainisha uungwaji mkono wa serikali kama juhudi za kuwawezesha vijana wa jimbo hilo kuhifadhi Qur'ani Tukufu
Akiwakilishwa na Spika wa Bunge la Ikulu ya Bauchi, Abubakar Sulaiman, gavana huyo alisema, "Historia ya Mashindano ya Kuhifadhi Qur'ani nchini Nigeria haiwezi kukamilika bila Jimbo la Bauchi kuzingatia utendaji wenyeji wa Jimbo hilo ambao wanafanya vyema katika mashindano mbalimbali ndani na nje ya nchi."
"Kwa hivyo, kuna haja ya kuendelea kusaidia shindano ili kuhimiza vizazi vya sasa na vijavyo," alisisitiza.
Gavana huyo ambaye aliwanashi washiriki wazingatie zaidi ya zawadi ambazo wanapata katika mashindano hayo ya Qur'an na badala yake wazingatia zaidi mafundiso ya Kitabu hicho Kitukufu
Mwenyekiti wa Kamati ya Jimbo la Mashindano ya Kuhifadhi Qur'ani Hassan Zango alipongeza uungwaji mkono wa mashindano hayo na kusema, "Kamati inajitahidi kuhakikisha haki inatendeka kwa washiriki ili serikali iendelee kufanya vyema katika ngazi za kitaifa na kimataifa."
Aliihakikishia kamati hiyo kujitolea kwa wote katika kufanikisha zoezi hilo.
Washiriki, waliotolewa kutoka maeneo yote ishirini ya serikali za mitaa za jimbo hilo, wanashindana katika kategoria sita za shindano hilo.
3490712