IQNA

Kongamano la Kimataifa la Qur'ani Tukufu lafanyika Tanzania

10:03 - May 22, 2025
Habari ID: 3480721
IQNA- Kongamano la 30 la Qur’an Tukufu na Hadithi limefanyika kwa mafanikio makubwa Jijini Dar-es-Salaam - Tanzania, likiwakutanisha wasomaji mahiri wa Qur’an kutoka nchini Iran na ndani ya Tanzania..

Kwa mujibu wa shirika la habari la ABNA, Kongamano hili liliandaliwa kwa ushirikiano wa taasisi mbalimbali zikiwemo: Chuo Kikuu Jamiat al-Mustafa (s) tawi la Tanzania chini ya uongozi wa Hujjatul Islam wal Muslimin, Dr. Ali Taqavi, Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT) ikiongozwa na Mwenyekiti wake Taifa, Sheikh Dr. Alhad Mussa Salum, Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) likiwa chini ya Mufti Mkuu wa Tanzania, Sheikh Dr. Abubakar Zubair bin Ally, pamoja na Kitengo cha Utamaduni wa Iran kinachoongozwa na Dr. Maarifi. Mgeni rasmi katika kongamano hilo alikuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mheshimiwa: Daniel Baran Sillo, ambaye katika hotuba yake aliwapongeza waandaaji na washiriki, huku akisisitiza nafasi ya Qur’an katika kuleta umoja, maadili na maendeleo ya Taifa. Akizungumza katika Kongamano hilo, Dr. Ali Taqavi aliwahimiza waumini wa Kiislamu kuendeleza juhudi za kusoma na kuelewa Qur’an kwa kina, kwa ajili ya kuleta Amani, Umoja Mshikamano na Ustawi wa Jamii ya Mwanadamu.

Miongoni mwa wasomaji Qur'ani walioshiriki kutoka Iran ni maqari wanaotambulika ambao ni Hamed Shakernejad na Ahmad Abolghasemi kutoka Iran. Wawili hao ni miongoni mwa wasomaji mashuhuri wa Qur’ani kutoka Iran na ni waongozaji wa kipindi maarufu cha  Mahfel kanali ya 3 ya televisheni ya Iran , ambacho kimepata watazamaji wengi duniani. Hivi karibuni, maqari hao wawili walishiriki katika mijumuiko mkiubwa ya Qur’ani nchini Indonesia.

Maqari wengine walio shiriki ni Sayed Jalal Masoomi, pia kutoka kipindi cha Mahfel TV, na maqari wawili mashuhuri wa Tanzania ambao Rajai Ayoub na Iddi Shaaban.

Vilevile, vijana wawili kutoka Iran, Mohammad Hossein Azimi na Mohanna Ghanbari, nao pia  wameshiriki katika hafla hiyo.

Tukio hili la kiroho limeendelea kuthibitisha nafasi ya Qur’an Tukufu kama dira ya maisha ya kijamii na kiroho, huku likiwa ni ishara ya mshikamano na ushirikiano miongoni mwa Waislamu ndani na nje ya Tanzania. Kongamano hilo pia limetajwa kuwa ni jukwaa la kukuza uelewa wa mafundisho ya Qur’an na kuimarisha mshikamano wa Kiislamu katika jamii.

  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
  • Qur'an - Dar
 

 

 

Habari zinazohusiana
captcha