IQNA

Mashhad inatarajiwa kupokea Milioni 15 kwa ajili ya mazishi ya Kiongozi Shahidi

15:00 - June 23, 2026
Habari ID: 3482394
IQNA – Gavana wa mji mtakatifu wa Mashhad, kaskazini mashariki mwa Iran amesisitiza utayari kamili wa mji huo katika kuandaa shughuli za mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Seyed Ali Khamenei.

Seyed Hassan Hosseini amesema kuwa anatarajia mahudhurio ya watu milioni 15 katika maandamano hayo ya mazishi.

Akizungumza katika kikao cha Baraza la Utawala la Mji wa Mashhad siku ya Jumatatu, alisema kuwa nchi nzima imejitayarisha kwa ajili ya tukio hili kubwa na la kihistoria la kumuaga Kiongozi huyo aliyekufa shahidi.

Alibainisha kuwa mji wa Mashhad umekuwa kitovu cha matukio mengi muhimu ya kihistoria, kisiasa, na kiutamaduni nchini Iran, na tukio hili litakuwa ni mgeuko muhimu katika historia ya mji huo.

“Sote tunapaswa kushirikiana ili shughuli hii ifanyike kwa namna bora zaidi. Kwa bahati njema, mji wa Mashhad una uwezo mkubwa wa kupokea watu, na ni wajibu wetu kuwakaribisha vyema mazuwari na wageni watakaohudhuria shughuli hii. Wageni hawa ni baraka kubwa kwa mji wa Mashhad, na kwa sasa asilimia 80 ya uwezo wa hoteli zetu tayari umeshajaa.”

Hosseini aliongeza, “Tutaisafisha na kuiandaa njia ya mazishi ipasavyo, na tunatabiri kuwa watu milioni 15 watahudhuria mazishi hayo. Ofisi ya Gavana inaunga mkono kikamilifu shughuli hii, na tumejiandaa na mahitaji yote muhimu kwa ajili ya kuwapokea wananchi.”

Alifafanua zaidi kuhusu malazi ya mazuwari, akisema kuwa mji huo umeandaa sehemu za malazi kwa ajili ya watu milioni 1.5, na “tuko tayari kuongeza uwezo huo. Tunatabiri kuwa mazuwari na wageni wa shughuli hii ya mazishi watakuwepo jijini kwa muda wa hadi wiki nzima. Hatujawahi kushuhudia uwepo wa idadi kubwa kama hii ya watu katika mji wa Mashhad hapo awali, hivyo tusishangae na tuwe tayari kuwahudumia kwa heshima.”

4359860

Habari zinazohusiana
captcha