
Kwa mujibu wa shirika rasmi la habari la Iran, IRNA, Masoud Pezeshkian, Rais wa Iran, ameandika kwenye mtandao wa X ujumbe ufuatao:
“Viongozi waheshimiwa wa nchi rafiki na majirani, tulijaribu, kwa msaada wenu na kupitia diplomasia, kuepuka vita. Lakini mashambulizi ya kijeshi ya Marekani na utawala wa Kizayuni hayajatuachia njia yoyote isipokuwa kujilinda.Tunaheshimu mamlaka yenu ya kujitawala na bado tunaamini kuwa utulivu wa eneo hili unapaswa kudhaminiwa na nchi za eneo zenyewe.”
Vikosi vya Majeshi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran vinaendeleza operesheni za ‘Ahadi ya Kweli 4’ ikiwa ni katika kujibu uchokozi wa Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel ulioanzishwa Jumamosi.
Operesheni hizo za kijeshi za Iran zimeendelea kulenga ngome za kijeshi, kiuchumi na kisiasa za utawala wa Kizayuni wa Israel na vituo vya kijeshi na kijasusi vya Marekani katika ardhi za nchi za eneo.
4338411