IQNA

Mashindano ya Qur'ani

Mashindano ya Kimataifa ya Qur’ani ya Iraq kufanyika Novemba

23:31 - August 30, 2024
Habari ID: 3479355
IQNA - Toleo la kwanza la Mashindano ya Kimataifa ya Qur'ani yaliyopewa jina la Tuzo la Qur'ani la Iraq yatafanyika katika mji mkuu wa nchi hiyo ya Kiarabu, Baghdad, mwezi wa Novemba.

Mashindano hayo yatapangwa kwa ushirikiano na mashirika ya Wakfu ya Shia na Sunni nchini Iraq. Washindani watashindana katika kategoria za kuhifadhi na usomaji wa Qur’ani Tukufu. Kikao cha kamati ya kiufundi ya mashirika ya Wakfu ya Shia na Sunni kilifanyika mjini Baghdad mapema wiki hii.

Baadhi ya maafisa wa kidini na wa Qur'ani na watu mashuhuri wa nchi hiyo pia walihudhuria mkutano huo. Walijadili maandalizi muhimu ya mashindano hayo ya kimataifa ya Qur'ani.

Toleo la kwanza la Tuzo la Kimataifa la Qur'ani la Iraq lilikuwa limepangwa kufanyika mapema 2024 lakini liliahirishwa kwa sababu kadhaa

Shughuli za Qur'ani zimeendelea kwa kiasi kikubwa nchini Iraq tangu kupinduliwa kwa dikteta wa zamani Saddam Hussein mwaka 2003.

Kumekuwa na mwelekeo unaokua wa programu za Qur'ani kama vile mashindano, vipindi vya kisomo na programu za elimu zilizofanyika nchini katika miaka ya hivi karibuni.

.

Iraq’s Int’l Quran Award Slated for November 

Iraq’s Int’l Quran Award Slated for November 

Iraq’s Int’l Quran Award Slated for November 

 

https://iqna.ir/en/news/3489693

Habari zinazohusiana
captcha