Kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki alitoa wito wa kusitishwa mara moja kwa mapigano kutokana na idadi kubwa ya wananchi wasiokuwa na hatia wanaoathirika.
Ametoa matamshi hayo wakati wa sala ya kila wiki ya Angelus katika Uwanja wa Mtakatifu Petro huko Vatican Kwa mujibu wa Papa Leo, dunia haina haki ya kubaki katika hali ya kutojali mateso ya raia.
“Hatuwezi kukaa kimya mbele ya mateso ya watu wengi, wahanga wasio na ulinzi wa mizozo hii. Kinachowaumiza wao, kinaumiza ubinadamu wote,” alisisitiza.
Papa Leo amesema kuwa matukio yanayoendelea Mashariki ya Kati yanamletea wasiwasi mkubwa.
Ameeleza kuwa anaendelea kufuatilia kwa tahadhari yanayojiri si tu katika eneo hilo, bali pia katika maeneo mengine ya dunia ambako vita na vurugu bado vinaendelea. Kilicho muhimu zaidi, kwa mujibu wake, ni kwamba mgogoro huo umekuwa wa muda mrefu na unaendelea kwa wiki kadhaa.
Kiongozi huyo wa Kanisa Katololiki amesisitiza tena mwito wake kwa jamii ya kimataifa kusitisha uhasama na kufungua njia ya suluhu ya amani.
“Naendelea kusisitiza kwa nguvu zote umuhimu wa kuomba kwa udumu ili mapigano yakome, na njia ya amani ifunguliwe hatimaye.”
3496854