iqna

IQNA

Kukabiliana na maadui wa Uislamu
TEHRAN (IQNA) - Yemen imepiga marufuku kuingia kwa bidhaa zinazozalishwa na nchi za Ulaya ambazo zimewezesha kuvunjiwa heshima Qur'ani Tukufu, ambapo kiongozi wa harakati ya muqawama ya Ansarullah ameitaja hatua wanayochukua kuwa ni "vikwazo vya kiuchumi".
Habari ID: 3476802    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/04/02

Sera za Kigeni Iran
TEHRAN (IQNA)- Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ametangaza kuwa, atakutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Saudi Arabia mnamo siku chache zijazo na akasema: "tulikubaliana kuwa jumbe za kiufundi za pande zote mbili zitembelee balozi na balozi ndogo na kufanya maandalizi ya kivitendo ya kufunguliwa tena balozi hizo."
Habari ID: 3476727    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/03/19

Uhusiano wa nchi za Kiislamu
TEHRAN (IQNA)- Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran amesisitiza stratejia isiyobadilika ya sera za nje za Jamhuri ya Kiislamu kuhusu ushirikiano wa pande zote, endelevu na wenye manufaa na maj iran i zake na kusema: ili kuondokana na changamoto zilizopo ambazo kuendelea kwake hakuna maslahi kwa nchi yoyote katika eneo hili, ni lazima ushirikiano na mshikamano vichuke nafasi ya mifarakano na uhasama.
Habari ID: 3476719    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/03/17

Khatibu wa Sala ya Ijumaa Tehran
TEHRAN (IQNA)- Khatibu wa Sala ya Ijumaa ya wiki hii mjini Tehran amesisitiza kuwa: adui amefanya makosa katika hesabu zake huku taifa la Iran likichagua mantikiya Mapinduzi ya Kiislamu.
Habari ID: 3476717    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/03/17

Sera za Kigeni
TEHRAN (IQNA)- Ofisi ya Uwakilishi wa Kudumu ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika mashirika ya kimataifa yaliyo na makao makuu yao mjini New York Marekani, imeandika kwa mnasaba wa Siku ya Kimataifa ya kupambana na Chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia) kwamba: "Iran inasisitiza mshikamano wake kamili na wahanga wa mashambulio yanayochochewa na chuki dhidi ya Uislamu kote duniani."
Habari ID: 3476716    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/03/16

Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran
TEHRAN(IQNA)-Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema: Leo hii ambapo maadui wanataka kuenenza fikra na mienendo ya ujahilia mamboleo katika jami, ni damu safi ya mashahidi ndiyo inayoondoa na kukabiliana na ujahilia huo.
Habari ID: 3476704    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/03/14

Ulimwengu wa Kiislamu
TEHRAN (IQNA)-Mhadhiri mwenye makao yake nchini Uingereza anasema Washington na Tel Aviv "zilishangazwa" baada ya Tehran na Riyadh kutangaza kuanzisha tena uhusiano wa kidiplomasia siku ya Ijumaa.
Habari ID: 3476698    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/03/12

Ulimwengu wa Kiislamu
TEHRAN (IQNA)- Makundi mbalimbali ya kieneo yamekaribisha makubaliano ya kurejesha tena uhusiano kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Ufalme wa Saudi Arabia.
Habari ID: 3476692    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/03/11

Ujumbe wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi kwa mataifa yanayozungumza Kihispania
TEHRAN (IQNA)- Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza katika salamu zake kwa mataifa yanayozungumza Kihispania juu ya kuzidi kujuana na kushirikiana mataifa yanayotetea haki na uadilifu.
Habari ID: 3476691    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/03/11

Ulimwengu wa Kiislamu
TEHRAN (IQNA)-Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Saudi Arabia zimefikia makubaliano ya kurejesha uhusiano wao wa kidiplomasia na kufungua tena balozi, miaka saba baada ya kuvunjika uhusiano huo kutokana na masuala kadhaa.
Habari ID: 3476685    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/03/10

Rais wa Ebrahim Raisi wa Iran
TEHRAN (IQNA)- Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema Iran iko tayari kuzipatia nchi za Afrika elimu na teknolojia mpya ili kurahisisha ushiriki wa sekta binafsi katika uhusiano wa pande mbili.
Habari ID: 3476678    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/03/08

Mashindano ya Qur'ani ya Iran
TEHRAN (IQNA) - Mtaalamu wa Qur'ani Tukufu kutoka Kuwait ambaye alikuwa katika jopo la majaji wa kitengo cha wanawake cha Mashindano ya 39 ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu ya Iran amesema mashindano hayo yanaweza kuwa mfano wa kuigwa na nchi zingine ambazo huandaa mashindano ya kimataifa ya Qur’ani Tukufu.
Habari ID: 3476619    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/02/24

Mashindano ya Qur'ani ya Iran
TEHRAN (IQNA) – Hafidh wa Qur’ani Tukufu kutoka Gambia amesifu kiwango kizuri na usawa alioushuhudia katika Mashindano ya 39 la Mashindano ya Kimataifa ya Qur’ani Tukufu ya Iran.
Habari ID: 3476617    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/02/24

Mazungumzo ya Uislamu na Ukristo
TEHRAN (IQNA) - Mkuu wa Shirika la Iran la Utamaduni na Mahusiano ya Kiislamu (ICRO) Hujjatul Islam Mohammad Mehdi Imanipour na Patriaki Kirill wa Moscow wamefanya mazungumzo katika mji mkuu wa Russia, Moscow.
Habari ID: 3476612    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/02/23

Rais wa Iran katika shehre za kufunga Mashindano ya Qur'ani
TEHRAN (IQNA) - Rais wa Iran Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu Iran amesema Iran inaweza kuwa mji mkuu wa kukuza utamaduni wa Qur'ani Tukufu duniani.
Habari ID: 3476610    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/02/23

Taazia
TEHRAN (IQNA)- Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amejiunga na maafisa wengine wa Iran katika kutoa mkono wa pole kufuatia kifo cha balozi wa miaka mingi na mkongwe wa Palestina, hapa nchini Iran. Balozi Salah al Zawawi alifariki dunia Jumatatu akiwa na umri wa miaka 85 katika hospitali moja ya hapa mjini Tehran.
Habari ID: 3476600    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/02/21

Mashindano ya Qur'ani
TEHRAN (IQNA) – Hafidh wa Qur'ani Tukufu kutoka Pakistani ambaye anashiriki katika fainali ya Mashindano ya 39 ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu ya Iran amesifu kiwango cha juu cha mashindano hayo.
Habari ID: 3476598    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/02/21

Mashindano ya Qur'ani ya Iran
TEHRAN (IQNA) – Mashindano ya 39 ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran yamefunguliwa rasmi Jumamosi Alasiri mjini Tehran.
Habari ID: 3476582    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/02/18

Kongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA)-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amezikosoa nchi za Kiislamu kwa kutochokua hatua yoyote ya maana juu ya kadhia ya Palestina.
Habari ID: 3476581    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/02/18

Mashindano ya Qur'ani Tukufu
TEHRAN (IQNA) - Hatua ya awali ya mashindano ya Qur'ani Tukufu kwa ajili ya wakimbizi wa Afghanistan wanaoishi nchini Iran ilifanyika katika mji mtakatifu wa wa Qom nchini Iran ambapo kulikuwa na washiriki 370.
Habari ID: 3476574    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/02/17