IQNA

Yemen yaapa kujibu mashambulizi ya Marekani ambayo yameua raia 24

9:39 - March 16, 2025
Habari ID: 3480380
IQNA – Harakati ya Ansarullah ya Yemen imeahidi kujibu uchokozi wa kijeshi wa hivi karibuni wa Marekani, kufuatia mashambulizi ya angani ya Marekani na Uingereza ambayo yalilenga maeneo kadhaa kote nchini, ikiwemo mji mkuu, Sanaa, na jimbo la kaskazini la Saada.

Kwa mujibu wa Wizara ya Afya ya Yemen, katika mashambulizi hayo dhidi ya mji mkuu wa Sana’a, ni maeneo ya raia tu yaliyolengwa. Wizara hiyo ililaani vikali mashambulizi hayo, ikiyataja kuwa “uhalifu wa kivita” na ukiukaji wa wazi wa sheria za kimataifa.

Kwa mujibu wa shirika la habari la Yemen, Saba, mashambulizi ya Marekani na Uingereza yaliendelea katika mkoa wa Sa'ada kaskazini-magharibi mwa Yemen.

Mashambulizi pia yalipiga maeneo ya al-Bayda na Hajjah, magharibi mwa Yemen, katika wilaya za Makiras na Qurayshiya, pamoja na wilaya ya Mubin katika Hajjah.

 Rais wa Marekani alitangaza kupitia X kwamba aliagiza shambulizi la kijeshi dhidi ya Ansarullah, ingawa mashambulizi hayo yalilenga raia wa Yemen.

Kwa mujibu wa uongozi wa Ansarullah, vikosi vya Yemen vilianza kushambulia maeneo muhimu ya Israel mnamo Oktoba 2023, kufuatia hatua za Israel kuzuia misaada muhimu kuingia Gaza. Kufuatia marufuku ya meli za Israeli kuvuka Bahari Nyekundu na maeneo mengine, Marekani, Uingereza na Israel zimekuwa zikishambulia raia na miundo ya kiraia ya Yemen kwa mabomu, huku vikosi vya Yemen vikijibu kwa kulenga mali za jeshi la majini la Marekani katika maji ya Yemen.

Katika taarifa baada ya mauaji ya Jumamosi, Baraza Kuu la Kisiasa la Ansarullah lilisema kuwa kulenga raia kunathibitisha udhaifu wa Marekani, huku likisisitiza kuwa "hili halitatuzuia kuunga mkono Gaza, badala yake litasababisha hali kuwa kali zaidi na yenye nguvu kubwa."

Taarifa hiyo imesema: "Tunawahakikishia watu wa Yemen waliothabiti na tunathibitisha kuwa wavamizi wataadhibiwa kwa njia ya kitaalamu na yenye uchungu."

Baraza hilo lilisema kuwa majibu yao yatafanya Marekani na utawala wa Israel kushindwa na kurudi nyuma kwa fedheha.

Wakati huohuo, baraza hilo liliitaka jumuiya ya kimataifa kutimiza wajibu wake mbele ya uchokozi huo wa Marekani na Israel, ambao lilisema “utakuwa na athari kwa wote.”

Kuhusu athari hizo, taarifa hiyo ilieleza kuwa mashambulizi ya anga ya Marekani dhidi ya Yemen yamerejesha hali ya kijeshi katika Bahari Nyekundu na kuibua tishio halisi kwa usalama wa safari za kimataifa za meli katika eneo hilo.

3492351

Habari zinazohusiana
Kishikizo: yemen ansarullah gaza
captcha