IQNA

Nakala Adimu ya ya Qur’ani Tukufu ya kurasa 60 yaonyeshwa Makka

15:28 - May 12, 2026
Habari ID: 3482231
IQNA – Msahafu adimu wenye kurasa 60 inaonyeshwa katika Makumbusho ya Qur’an Tukufu yaliyo katika Eneo la Kitamaduni la Hira, mjini Makka.

Katika nakala hii ya kipekee, kila ukurasa una hizb moja kamili ya Qur'ani Tukufu. Msahafu huo umeandikwa kwa umakini mkubwa na ustadi wa hali ya juu wa kisanaa, na umechapishwa na taasisi ya uchapishaji ya Tunisia, ukiakisi namna Waislamu walivyoihifadhi na kuisitiri Qur’an Tukufu katika zama mbalimbali.

Nakala hii inaonesha juhudi za kihistoria zilizofanywa kwa ajili ya kuhifadhi na kuwasilisha Qur’ani kwa mitindo ya kipekee ya kisanaa, huku ikiangazia uzuri wa kaligrafia ya Kiarabu na mpangilio wa maandishi ya Qur’ani Tukufu.

Inaonyeshwa kama sehemu ya mkusanyiko wa maonyesho ya kihistoria wa makumbusho hayo, pamoja na teknolojia shirikishi zilizowekwa ili kuboresha tajriba ya wageni.

Makumbusho hayo yanaonesha maendeleo ya uandishi wa Qur’ani katika historia ya Uislamu ndani ya mazingira ya kielimu yanayoakisi hadhi ya Makka kama mahali pa kushukia wahyi.

3497416

Habari zinazohusiana
captcha