Indhari hiyo imetolewa na shirika la Umoja wa Mataifa la wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA) ambalo katika taarifa iliyotumwa kwenye Facebook siku ya Jumatano, ilisema familia kote Gaza "ziko ukingoni kufa kutokana na kiu" huku mifumo ya maji ikiporomoka kutokana na mashambulizi yanayoendelea ya Israel na kizuizi cha petrol ambacho kimekuwepo tangu Machi.
"Ni 40% tu ya vifaa vya uzalishaji wa maji ya kunywa bado vinafanya kazi," shirika hilo lilisema. "Gaza iko kwenye ukingo wa ukame unaosababishwa na mwanadamu."
Shirika hilo liliongeza kuwa uwezo wake wa kusambaza maji umepungua hadi nusu ya kiasi kilichotolewa wakati wa usitishaji vita wa mwisho ambao ulikiukwa na Israel katikati ya mwezi Machi.
Mwezi uliopita, manispaa kote eneo hilo zilionya kuwa hazikuweza kudumisha huduma za kimsingi, ikiwa ni pamoja na uendeshaji wa visima vya maji, kwa sababu ya uhaba wa mafuta.
Kwa mujibu wa ofisi ya vyombo vya habari vya serikali ya Gaza, vikosi vya Israel vimeharibu au kutofanya kazi visima 719 vya maji tangu Oktoba 2023, na kusababisha shida kubwa ya maji.
Pedro Arrojo-Agudo, ripota maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu kwa maji salama ya kunywa na usafi wa mazingira, alisema mwezi uliopita kwamba uharibifu wa Israel wa miundombinu ya maji ya Gaza na kunyimwa maji safi ni sawa na "bomu kimya lakini hatari."
Gaza imekabiliwa na janga la kibinadamu linalozidi kuwa mbaya tangu Israel ilipofunga vivuko vya mpaka Machi 2, na kuzuia kuingia kwa chakula, dawa, misaada ya kibinadamu na mafuta, huku ikizidisha mauaji yake ya kimbari katika eneo lililozingirwa.
Likikataa wito wa kimataifa wa kusitisha mapigano, jeshi la Israel limeendesha mashambulizi ya kikatili nay a mauaji ya kimbari dhidi ya Gaza tangu Oktoba 2023, na hadi sasa utawala huo umeua zaidi ya Wapalestina 56,000 wengi wao wakiwa wanawake na watoto.
3493593/